RAI YATOLEWA KWA WANANCHI KINONDONI KUSHIRIKI KWA PAMOJA KUANGAMIZA MAZALIA YA MBU, ILI KUWEZA KUJIKINGA NA UGONJWA WA DENGUE Posted On: July 4th, 2019 Rai hiyo imetolewa leo na Waziri wa Afya, Maendeleo ya jamii, jinsia wazee na watoto Mhe. Ummy Mwalimu katika ziara yake Manispaa ya Kinondoni kwa lengo la kushiriki zoezi la unyunyuziaji wa viuadudu (biolarvicides) kwa mazalia ya mbu ikiwa ni sehemu ya kuunga mkono zoezi la uhamasishaji wa udhibiti wa ugonjwa huo katika Wilaya hiyo. Amesema swala la uwajibikaji udhibiti wa mazalia haya ya mbu ni ya kila mwananchi, kwani kwa kufanya hivyo kutasaidia si tu kuondokana na ugonjwa wa Dengue, bali pia magonjwa mengine kama vile Malaria, zika, matende, Atikungunya na homa ya manjano. Amesema "Kwanza niipongeze Manispaa ya Kinondoni kwa kuonesha jitihada za kuhakikisha wanadhibiti ugonjwa huu wa Dengue kwa kununua mashine na viuadudu hivi ambavyo leo tunapulizia dawa, katika kupambana na mazalia ya mbu lakini pia niwapongeze kwa kupunguza idadi ya wagonjwa wapya wa homa ya Dengue kutoka 45 kwa siku mwezi April mpaka kufikia wagonjwa 17 kwa siku mwezi June" Waziri Ummy. Naye Mkuu wa wilaya ya Kinondoni Mhe Daniel Chongolo amesema Kinondoni imeshafikia asilimia 70 ya maeneo yake kwa kupulizia dawa ya kuua mazalia ya mbu kwa kutumia vikundi vya jamii vinavyopita mtaani na kubainisha hatua ambazo tayari zimeshakuliwa kuendelea kudhibiti mazalia haya ya mbu ambayo ni uagizaji wa mashine maalum za upuliziaji hewani (Fog machine) ambazo zitawezesha kupuliza dawa eneo kubwa zaidi kwa muda mchache. Aidha Mganga Mkuu wa Manispaa ya Kinondoni Dkt Festo Dugange katika nafasi yake amewataka wananchi mara waonapo dalili za homa ya dengue kuwahi kituo cha afya ili waweze kupata matibabu stahiki na kuachana na tiba za mtaani kama majani ya mpapai na mafuta ya nazi. Zoezi hilo la upuliziaji viuadudu vya kuua mazalia ya mbu limehudhuriwa pia na Mbunge wa Kinondoni Mh Maulid Mtulia, Mstahiki Meya wa Manispaa hiyo Mhe. Benjamin Sitta, Mkurugenzi wa Manispaa Ndg Aron Kagurumjuli na wakazi wa Eneo la Mwananyamala. Imeandaliwa na Kitengo Cha Habari na Uhusiano Manispaa ya Kinondoni. RAI YATOLEWA KWA WANANCHI KINONDONI KUSHIRIKI KWA PAMOJA KUANGAMIZA MAZALIA YA MBU, ILI KUWEZA KUJIKINGA NA UGONJWA WA DENGUE Posted On: ... + Read more »
KINONDONI YAUNDA BARAZA LA WAZEE LA WILAYA Posted On: June 21st, 2019 Baraza hilo lenye wajumbe saba akiwemo Mwenyekiti na msaidizi, Katibu na Msaidizi wake, mtunza fedha na wawakilishi wawili, limeundwa kwa uchaguzi uliofanyika kwa wazee wawakilishi kutoka kata 20, za Manispaa hiyo kupiga kura katika kikao kilichofanyika katika moja ya kumbi za Kanisa katoliki Manzese. Akiongoza zoezi hilo, kwa niaba ya Maganga Mkuu wa Manispaa ya Kinondoni, Bi Nusura Kessy amesema, wazee ni hazina ya Taifa, hivyo yapaswa kupaza sauti juu ya maswala yanayowahusu na kuwasemea haki zao za Msingi pale inapobidi ili waweze kutatuliwa. "Wazee ni hazina ya Taifa, nilazima walindwe, waheshimiwe watunzwe, na mashauri yao yasikilizwe, hivyo kwa baraza hili la wazee wa Wilaya mtakaloliunda kwa kufanya uchaguzi huru na wa haki unaozingatia vigezo leo, mtakuwa mmejitendea haki lakini pia baraza hilo likawe kisemeo katika yale yanayowapasa kusema " Bi. Nusura Kessy. Awali akitaja majukumu ya baraza hilo la wazee la Wilaya, Bi. Judith Kimaro ambaye pia ni mkuu wa Kitengo cha ustawi wa jamii amesema Baraza linalo majukumu yake ya msingi ambayo ni kupitia majumuisho ya kero za wazee zilizoletwa na wawakilishi, kufanya mkutano wa baraza la wazee la Wilaya kila baada ya miezi mitatu, kuwasilisha kero za wazee kwenye baraza la madiwani, kuchagua wawakilishi wawili kwenye baraza la madiwani, kushawishi Halmashauri kutenga bajeti kwa ajili ya miradi ya uzalishaji ya wazee pamoja na kuratibu mabaraza ya wazee ya Kata. Naye mratibu wa wazee Manispaa ya Kinondoni Bi Neema Mwalubilo alipokuwa akitoa taarifa ya hali ya wazee Manispaa ya Kinondoni amesema ni ya kiridhisha kwani wameweza kuunganishwa kwenye huduma za afya kwa kutengenezewa vitambulisho takribani 11,340 vya msamaha . Aidha ameainisha mikakati iliyopo ya kuinua hali ya wazee katika Manispaa hiyo kuwa ni kuhakikisha wote wanapata kadi za matibabu, kuwaongezea na kuwajengea uwezo wa kujikwamua kiuchumi pamoja na kuwaunganisha na wadau mbalimbali kwa ajili ya misaada. Imeandaliwa na Kitengo cha Habari na Uhusiano. Manispaa ya Kinondoni. KINONDONI YAUNDA BARAZA LA WAZEE LA WILAYA Posted On: June 21st, 2019 Baraza hilo lenye wajumbe saba akiwemo Mwenyekiti na msaidizi, K... + Read more »
TAMISEMI YARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA DMDP NA TARURA KINONDONI. Posted On: June 21st, 2019 Hayo yamethibitika leo wakati Waziri wa TAMISEMI Mhe. Suleiman Jafo alipofanya ziara ya ukaguzi wa miradi hiyo kwa lengo la kujiridhisha na ubora wake ikiwa ni pamoja na kuangalia hatua za utekelezaji zilizofikwa. Amesema utekelezaji wa miradi hii kwa mkoa wa Dar es salaam ni ya muhimu sana kwani itatatua kero kubwa walizokuwa wakizipata wananchi hasa yale maeneo waliyokuwa wakisumbuliwa na mafuriko na zile zilizokuwa na uharibifu mkubwa. "Miradi hii ni muhimu sana kwani inaenda kubadilisha sura ya Dar es salaam, tunachotaka kama Serikali ni kuhakikisha kero kwa wananchi zinaondolewa na hata wale walioko masomoni wakirudi, tuwashike mikono, taswira ibadilike "Amesisitiza Jafo. Naye Mratibu wa DMDP Manispaa ya Kinondoni Ndg. Mkelewe Tungaraza alipokuwa akitoa taarifa ya utekelezaji wa miradi ya DMDP amesema dhamira yao kubwa ni kuhakikisha wanaisimamia na kuitekeleza kwa kiwango kinachotakiwa ili ilete tija kwa wananchi husika. Katika hatua nyingine, Waziri Jafo amewataka wananchi kuhakikisha wanazitunza na kuzifanyia usafi barabara hizo, ikiwa ni pamoja na kuepuka kutupa taka kwenye mitaro kwani kwa kufanya hivyo kutaathiri ubora na Mazingira kwa ujumla. Kadhalika amewataka wakandarasi kuhakikisha wanakamilisha suala la uwekaji wa alama za barabara hizo,, ikiwa ni pamoja na kufanya kazi kwa weledi, kwa kuzingatia vigezo na viwango vya ubora ili miundombinu hiyo iweze kudumu kwa muda mrefu huku ikiendelea kusaidia wananchi. Katika ziara hiyo aliyotembelea barabara ya Mbezi Makonde, Kilongawima, akachube na makanya pia imehudhuriwa na wakuu wa wilaya ya Ubungo na Kinondoni, wakurugenzi, wakandarasi pamoja na waratibu wa TARURA na DMDP. Imeandaliwa na Kitengo cha Uhusiano na Habari. Manispaa ya Kinondoni. TAMISEMI YARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA DMDP NA TARURA KINONDONI. Posted On: June 21st, 2019 Hayo yamethibitika leo wakati Waz... + Read more »
KUELEKEA KILELE CHA SIKU YA MTOTO WA AFRICA, KINONDONI YAADHIMISHA KWA VITENDO Posted On: June 14th, 2019 Kuelekea siku ya kilele cha Mtoto wa Afrika chenye kauli mbiu isemayo "Mtoto ni msingi wa Taifa endelevu tumutunze, tumlinde na kumuendeleza", Kinondoni yaadhimisha kwa kutoa zawadi mbalimbali kwa watoto wenye uhitaji maalumu pamoja na michezo. Akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni katika sherehe hizo zilizofanyika Kiwilaya katika shule ya msingi Magomeni, Katibu Tawala wa Wilaya hiyo Bi. Stella Msofe amesema watoto ni hazina ya Taifa, hivyo wanapaswa kulindwa, kutunzwa, kuthaminiwa, kuheshimiwa na kubwa zaidi kuwapatia haki za msingi kama elimu na afya. Ameongeza kuwa wakati umefika wa Serikali kutofumbia macho unyanyapaa wa watoto wenye mahitaji maalumu hususani ulemavu wa viungo vya mwili kwani wanayo haki na nafasi sawa katika jamii, hivyo wapewe nafasi wanayostahili na kupatiwa vipaumbele kama watoto kwani ndio warithi wa baadae wa Taifa hili. "Leo hii Tanzania tunajivunia maendeleo yanayosimamiwa na Mh Rais Dr. John Pombe Joseph Magufuli, naye aliwahi kuwa mtoto akakuwa, akatunzwa akapewa haki zake, na leo hii ndiye kiongozi shupavu, yote hii ni kwasabababu aliandaliwa vema mpaka amekuwa na uwezo huo na sisi kama jamii tukitenda haki sawa kwa kuwathamini wote bila kujali hali zao, tutakuwa tunaandaa viongozi bora wa baadae" amesisitiza Bi Stella. Naye Bi. Halima Kahema ambaye ni Mkuu wa Idara ya idara ya maendeleo ya jamii katika Manispaa hiyo akiongea kwa niaba ya Mkurugenzi amesema Manispaa yake iko tayari kushirikiana na Asas hizi katika kuhakikisha haki ya mtoto inatekelezwa na wahitaji wananufaika nayo. Katika maadhimisho hayo yaliyoambatana na utoaji wa vyeti vya ushiriki za Asas sita, pamoja na zawadi za madaftari na fulana kwa watoto, pia yalipambwa na michezo ya kukimbia, kuruka kamba na kukimbiza kuku . Asas zilizoshiriki katika maadhimisho hayo ni Kihowede, AHRN, Save the children, PDF (peopale development forum), Red cross na Tiba. Imeandaliwa na Kitengo Cha Habari na Uhusiano Manispaa ya Kinondoni KUELEKEA KILELE CHA SIKU YA MTOTO WA AFRICA, KINONDONI YAADHIMISHA KWA VITENDO Posted On: June 14th, 2019 Kuelekea siku ya kilele cha M... + Read more »
KINONDONI YASAINI MIKATABA NA MAKAMPUNI MAWILI YA TAKRIBANI BILIONI 58 Posted On: June 13th, 2019 NI KWA AJILI YA UJENZI NA MABORESHO YA MTO NG'OMBE NA BARABARA YA SHEKILANGO KWA KIWANGO CHA NJIA NNE. Akisaini mikataba hiyo, kati yake na makampuni hayo, Mkurugenzi wa Manispaa ya Kinondoni Ndg. Aron Kagurumjuli amesema, mradi wa mto ng'ombe utakaogharimu bilioni 32, utajengwa na kampuni ya China Henan International Cooperation Group CO. LTD na mradi wa barabara ya shekilango wa njia nne utakaogharimu shilingi 26 bilioni, utajengwa na Kampuni ya China road and bridge Cooperation hali itakayosaidia si tu kuboresha maeneo hayo bali pia kuyapandisha hadhi kwa kiwango kusudiwa. Amesema katika mikataba hiyo pia yatajengwa mabwawa ya kukusanyia maji eneo la karibu na chuo cha maji kutoka maeneo mbalimbali na maji hayo yataruhusiwa kuingia taratibu mto ng'ombe hali ambayo itasaidia kupunguza mafuriko. Akishuhudia utilianaji sahihi mikataba hiyo, Mstahiki Meya Wa Manispaa ya Kinondoni Mhe. Benjamini Sitta amesema, Serikali ya awamu ya tano ni Serikali sikivu yenye lengo la kuboresha makazi duni na kuwatoa wananchi kwenye kifungo cha mateso ya mafuriko, na ujenzi huu wa mto ng'ombe utasaidia kwa kiasi kikubwa kupunguza kadhia hiyo iliyokuwa ikisumbua wananchi wa maeneo ya Tandale na kijitonyama. Aidha Meya Sitta pia amewataka makandarasi wanaojenga miradi hiyo kujenga kwa wakati na kwa ubora stahiki ili waweze kumaliza kero iliyokuwa inawasumbua wananchi kwa muda mrefu. Imeandaliwa na Kitengo Cha Habari na Uhusiano Manispaa ya Kinondoni. KINONDONI YASAINI MIKATABA NA MAKAMPUNI MAWILI YA TAKRIBANI BILIONI 58 Posted On: June 13th, 2019 NI KWA AJILI YA UJENZI NA MABORESHO Y... + Read more »
ELIMU YA AFYA, UZAZI NA UPIMAJI NA USHAURI NASAHA KWA WANANCHI YATOLEWA KINONDONI. Posted On: June 7th, 2019 Kinondoni kwa kushirikiana na shirika lisilo la kiserikali la JHPIEGO lenye kauli mbiu ya "TUPANGE PAMOJA"yaendesha zoezi la utoaji elimu ya Afya ya Uzazi, upimaji na ushauri nasaha kwa wananchi ili kulinda na kuboresha afya zao. Akifafanua kuhusu zoezi hilo, lililofanyika katika mtaa wa Hananasif Kinondoni, Mganga Mkuu wa Manispaa hiyo Dr Festo Ndugange amesema kuwa kipaumbele cha serikali ya awamu ya tano ni kujenga na kukuza uchumi wa nchi kupitia Viwanda, katika kuhakikisha hilo linatimia wanahitajika watu wenye afya njema kimwili na kiakili ili waweze kutoa mchango utakiwao kwa wakati sahihi. "Wakati viongozi wetu wanapigania masuala ya kukuza uchumi wanahitaji mwitikio chanya kutoka kwenye jamii na hilo linawezekana endapo jamii hiyo itakuwa na watu wenye afya njema na nguvu imara, nasi tumeona namna nzuri ya kutoa mchango wetu ni kuwapa elimu, kinga na tiba imara wakati wote" ameongeza Dr Festo. Akiongea katika zoezi hilo, mratibu wa huduma ya afya ya uzazi na mtoto Manispaa ya Kinondoni Bi. Edith Manase Mboga amesema, huduma na elimu inayotolewa inalenga kupunguza au kumaliza kabisa matatizo yanayoikumba jamii hasa ikizingatiwa chanzo chake ni ukosefu wa uelewa na kutokuwa na uthubutu wa familia kukaa na kuweka mikakati ya pamoja juu ya masuala ya afya. Huduma walizopatiwa wananchi hao ni elimu juu ya afya ya uzazi, upimaji wa saratani ya shingo ya kizazi na matiti, shinikizo la damu, ushauri nasaha na upimaji wa hiari wa VVU. Wananchi waliojitokeza katika zoezi hilo wameishukuru Manispaa ya Kinondoni kwa fursa hiyo adimu itakayowawezesha kupata elimu juu ya mwasuala ya Afya ya uzazi pamoja na athari azipatazo mtu asiyefuata masuala hayo ya Afya. Imeandaliwa na Kitengo Cha Habari na Uhusiano Manispaa ya Kinondoni. ELIMU YA AFYA, UZAZI NA UPIMAJI NA USHAURI NASAHA KWA WANANCHI YATOLEWA KINONDONI. Posted On: June 7th, 2019 Kinondoni kwa kushirikiana... + Read more »
ELIMU YA AFYA, UZAZI NA UPIMAJI NA USHAURI NASAHA KWA WANANCHI YATOLEWA KINONDONI. Posted On: June 7th, 2019 Kinondoni kwa kushirikiana na shirika lisilo la kiserikali la JHPIEGO lenye kauli mbiu ya "TUPANGE PAMOJA"yaendesha zoezi la utoaji elimu ya Afya ya Uzazi, upimaji na ushauri nasaha kwa wananchi ili kulinda na kuboresha afya zao. Akifafanua kuhusu zoezi hilo, lililofanyika katika mtaa wa Hananasif Kinondoni, Mganga Mkuu wa Manispaa hiyo Dr Festo Ndugange amesema kuwa kipaumbele cha serikali ya awamu ya tano ni kujenga na kukuza uchumi wa nchi kupitia Viwanda, katika kuhakikisha hilo linatimia wanahitajika watu wenye afya njema kimwili na kiakili ili waweze kutoa mchango utakiwao kwa wakati sahihi. "Wakati viongozi wetu wanapigania masuala ya kukuza uchumi wanahitaji mwitikio chanya kutoka kwenye jamii na hilo linawezekana endapo jamii hiyo itakuwa na watu wenye afya njema na nguvu imara, nasi tumeona namna nzuri ya kutoa mchango wetu ni kuwapa elimu, kinga na tiba imara wakati wote" ameongeza Dr Festo. Akiongea katika zoezi hilo, mratibu wa huduma ya afya ya uzazi na mtoto Manispaa ya Kinondoni Bi. Edith Manase Mboga amesema, huduma na elimu inayotolewa inalenga kupunguza au kumaliza kabisa matatizo yanayoikumba jamii hasa ikizingatiwa chanzo chake ni ukosefu wa uelewa na kutokuwa na uthubutu wa familia kukaa na kuweka mikakati ya pamoja juu ya masuala ya afya. Huduma walizopatiwa wananchi hao ni elimu juu ya afya ya uzazi, upimaji wa saratani ya shingo ya kizazi na matiti, shinikizo la damu, ushauri nasaha na upimaji wa hiari wa VVU. Wananchi waliojitokeza katika zoezi hilo wameishukuru Manispaa ya Kinondoni kwa fursa hiyo adimu itakayowawezesha kupata elimu juu ya mwasuala ya Afya ya uzazi pamoja na athari azipatazo mtu asiyefuata masuala hayo ya Afya. Imeandaliwa na Kitengo Cha Habari na Uhusiano Manispaa ya Kinondoni. ELIMU YA AFYA, UZAZI NA UPIMAJI NA USHAURI NASAHA KWA WANANCHI YATOLEWA KINONDONI. Posted On: June 7th, 2019 Kinondoni kwa kushirikiana... + Read more »