KINONDONI KUENDELEZA KIWANJA NA.1024 MWENGE KIHUDUMA NA KIBIASHARA KWA KUJENGA KITUO CHA MABASI Posted On: September 11th, 2019 Hayo yameelezwa leo na Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Mhe.Daniel Chongolo alipokutana na wafanyabiashara wa eneo hilo la Mwenge na kuzungumza nao katika kikao kilichofanyika ukumbi wa mikutano wa Manispaa. Amesema kwa kufanya hivyo ni kwenda sambamba na utekelezaji wa ilani ya Chama cha Mapinduzi inayosisitiza suala zima la uboreshaji wa miundombinu katika nyanja mbalimbali ikiwemo huduma za jamii kwa wamachinga na wafanyabiashara katika shughuli zao za kujipatia kipato na kukuza uchumi wao. "Sisi tunamuongozo unaoitwa ilani ya Chama cha Mapinduzi, kwenye ilani hiyo inasema wazi kabisa kwa kipindi cha miaka mitano tunaweka mazingira rafiki kabisa kwa wafanyabiashara yakihusisha maeneo ya biashara, mtaji na uhakika wa eneo hivyo hatuna budi kuhakikisha hilo ambalo lipo ndani ya uwezo wetu linafanikiwa" Amefafanua Chongolo. Aidha amefafanua kuwa uendelezaji huo utahusisha ujenzi wa maduka ya kati ya kibiashara(min- supermarket), sehemu za mamalishe, maduka ya rejareja, maduka ya spea za magari, saluni, vituo vya tax na bajaji, migahawa, vyoo vya jumuiya pamoja na huduma nyingine. Kadhalika amewataka wakazi na wafanyabiashara wanaofanya shughuli zao katika eneo la kiwanja1024 kuwa sehemu ya uendelezaji huo kwa kutoa ushirikiano pale inapopasa ili kwa pamoja turahisishe maendeleo yenye tija kwa biashara zetu na Taifa kwa ujumla. Alipokuwa akiongea mfanyabiashara mmoja kwa niaba ya wengine ameonesha kuupokea mradi huo na kuahidi kushirikiana na Serikali katika kuhakikisha unafanikiwa kwa kiwango chenye tija na kilichokusudiwa, na kuiomba serikali iwafikirie pia mara baada ya kukamilika kwake wawe wakwanza kupatiwa maeneo kwa ajili ya kufanyia biashara. Imeandaliwa na Kitengo cha habari na uhusiano Manispaa ya Kinondoni KINONDONI KUENDELEZA KIWANJA NA.1024 MWENGE KIHUDUMA NA KIBIASHARA KWA KUJENGA KITUO CHA MABASI Posted On: September 11th, 2019 Hayo ya... + Read more »
KINONDONI YAPOKEA MSAADA WA SAMANI ZA SHULE KUTOKA KWA INTERNATIONAL SCHOOL OF TANGANYIKA Posted On: September 6th, 2019 Akipokea msaada huo kutoka kwa Mkurugenzi wa IST Dr. Mark Hardeman, Mstahiki Meya Manispaa ya Kinondoni Mhe.Benjamini Sita amesema samani hizi zimekuja wakati ambao Serikali yetu ya awamu ya tano inasisitiza ubora wa miundombinu ya elimu, inayoenda sambamba na ushirikiano wa kielimu baina ya shule na shule kwa lengo la kukuza ujuzi katika kufundisha. Amesema suala la elimu nchini Tanzania limechukua sura ya kipekee hali inayopelekea viongozi kuwa wabunifu katika kuhakikisha wanaendana na sera ya elimu bora na kubainisha kuwa Kinondoni tayari wamejipanga vizuri katika kuhakikisha wanatekeleza upatikanaji wa elimu bora na sio bora elimu. "Katika kuhakikisha tunaendana na kasi ya Mhe. Rais tunatakiwa kuwa wabunifu kila iitwapo leo, leo hii tumepata samani kwa ajili ya shule zetu mbili za Mbweni Teta na Kigogo pamoja na vitabu zaidi ya boksi 44 na tumefanikiwa kupata vifaa hivi kwa kuwa na ushirikiano mzuri na wenzetu wa International School of Tanganyika, hata hivyo tunarajia kupokea vifaa vingi zaidi." Ameongeza Meya. Aidha Msitahiki Meya amesema kuwa upo mfumo mpya ambao anatarajia kuutambulisha hivi karibuni ambao utakuwa chachu ya mafanikio ya elimu kwa Manispaa yake ambacho kitaweza kuinufaisha Nchi kwa ujumla. Naye Dr. Mark Hardeman kutoka International School of Tanganyika amesema kuwa ushirikiano uliopo baina ya Taasisi yake na Manispaa ya Kinondoni ni wa kipekee sana na ameahidi kudumisha na kunufaisha sekta mbalimbali zilizopo na zitakazobuniwa wakati wowote. Kadhalika Afisa Elimu Sekondari Manispaa ya Kinondoni Mwl. Leonard Msigwa kwa niaba ya Mkurugenzi wa Manispaa ya Kinondoni ameishukuru Taasisi hiyo ya shule kwa kuonesha ushirikiano wenye manufaa zaidi tena kwa mda muafaka . Imeandaliwa na Kitengo Cha Uhusiano na Habari Manispaa ya Kinondoni. KINONDONI YAPOKEA MSAADA WA SAMANI ZA SHULE KUTOKA KWA INTERNATIONAL SCHOOL OF TANGANYIKA Posted On: September 6th, 2019 Akipokea msaad... + Read more »