ELIMU YA AFYA, UZAZI NA UPIMAJI NA USHAURI NASAHA KWA WANANCHI YATOLEWA KINONDONI. Posted On: June 7th, 2019 Kinondoni kwa kushirikiana na shirika lisilo la kiserikali la JHPIEGO lenye kauli mbiu ya "TUPANGE PAMOJA"yaendesha zoezi la utoaji elimu ya Afya ya Uzazi, upimaji na ushauri nasaha kwa wananchi ili kulinda na kuboresha afya zao. Akifafanua kuhusu zoezi hilo, lililofanyika katika mtaa wa Hananasif Kinondoni, Mganga Mkuu wa Manispaa hiyo Dr Festo Ndugange amesema kuwa kipaumbele cha serikali ya awamu ya tano ni kujenga na kukuza uchumi wa nchi kupitia Viwanda, katika kuhakikisha hilo linatimia wanahitajika watu wenye afya njema kimwili na kiakili ili waweze kutoa mchango utakiwao kwa wakati sahihi. "Wakati viongozi wetu wanapigania masuala ya kukuza uchumi wanahitaji mwitikio chanya kutoka kwenye jamii na hilo linawezekana endapo jamii hiyo itakuwa na watu wenye afya njema na nguvu imara, nasi tumeona namna nzuri ya kutoa mchango wetu ni kuwapa elimu, kinga na tiba imara wakati wote" ameongeza Dr Festo. Akiongea katika zoezi hilo, mratibu wa huduma ya afya ya uzazi na mtoto Manispaa ya Kinondoni Bi. Edith Manase Mboga amesema, huduma na elimu inayotolewa inalenga kupunguza au kumaliza kabisa matatizo yanayoikumba jamii hasa ikizingatiwa chanzo chake ni ukosefu wa uelewa na kutokuwa na uthubutu wa familia kukaa na kuweka mikakati ya pamoja juu ya masuala ya afya. Huduma walizopatiwa wananchi hao ni elimu juu ya afya ya uzazi, upimaji wa saratani ya shingo ya kizazi na matiti, shinikizo la damu, ushauri nasaha na upimaji wa hiari wa VVU. Wananchi waliojitokeza katika zoezi hilo wameishukuru Manispaa ya Kinondoni kwa fursa hiyo adimu itakayowawezesha kupata elimu juu ya mwasuala ya Afya ya uzazi pamoja na athari azipatazo mtu asiyefuata masuala hayo ya Afya. Imeandaliwa na Kitengo Cha Habari na Uhusiano Manispaa ya Kinondoni. ELIMU YA AFYA, UZAZI NA UPIMAJI NA USHAURI NASAHA KWA WANANCHI YATOLEWA KINONDONI. Posted On: June 7th, 2019 Kinondoni kwa kushirikiana... + Read more »
ELIMU YA AFYA, UZAZI NA UPIMAJI NA USHAURI NASAHA KWA WANANCHI YATOLEWA KINONDONI. Posted On: June 7th, 2019 Kinondoni kwa kushirikiana na shirika lisilo la kiserikali la JHPIEGO lenye kauli mbiu ya "TUPANGE PAMOJA"yaendesha zoezi la utoaji elimu ya Afya ya Uzazi, upimaji na ushauri nasaha kwa wananchi ili kulinda na kuboresha afya zao. Akifafanua kuhusu zoezi hilo, lililofanyika katika mtaa wa Hananasif Kinondoni, Mganga Mkuu wa Manispaa hiyo Dr Festo Ndugange amesema kuwa kipaumbele cha serikali ya awamu ya tano ni kujenga na kukuza uchumi wa nchi kupitia Viwanda, katika kuhakikisha hilo linatimia wanahitajika watu wenye afya njema kimwili na kiakili ili waweze kutoa mchango utakiwao kwa wakati sahihi. "Wakati viongozi wetu wanapigania masuala ya kukuza uchumi wanahitaji mwitikio chanya kutoka kwenye jamii na hilo linawezekana endapo jamii hiyo itakuwa na watu wenye afya njema na nguvu imara, nasi tumeona namna nzuri ya kutoa mchango wetu ni kuwapa elimu, kinga na tiba imara wakati wote" ameongeza Dr Festo. Akiongea katika zoezi hilo, mratibu wa huduma ya afya ya uzazi na mtoto Manispaa ya Kinondoni Bi. Edith Manase Mboga amesema, huduma na elimu inayotolewa inalenga kupunguza au kumaliza kabisa matatizo yanayoikumba jamii hasa ikizingatiwa chanzo chake ni ukosefu wa uelewa na kutokuwa na uthubutu wa familia kukaa na kuweka mikakati ya pamoja juu ya masuala ya afya. Huduma walizopatiwa wananchi hao ni elimu juu ya afya ya uzazi, upimaji wa saratani ya shingo ya kizazi na matiti, shinikizo la damu, ushauri nasaha na upimaji wa hiari wa VVU. Wananchi waliojitokeza katika zoezi hilo wameishukuru Manispaa ya Kinondoni kwa fursa hiyo adimu itakayowawezesha kupata elimu juu ya mwasuala ya Afya ya uzazi pamoja na athari azipatazo mtu asiyefuata masuala hayo ya Afya. Imeandaliwa na Kitengo Cha Habari na Uhusiano Manispaa ya Kinondoni. ELIMU YA AFYA, UZAZI NA UPIMAJI NA USHAURI NASAHA KWA WANANCHI YATOLEWA KINONDONI. Posted On: June 7th, 2019 Kinondoni kwa kushirikiana... + Read more »
WADAU NA JAMII KWA UJUMLA WAMETAKIWA KUONESHA UPENDO KWA KUWAKUMBUKA NA KUWAJALI WATU WENYE UHITAJI MAALUMU KATIKA JAMII. Posted On: May 31st, 2019 Hayo yamebainika leo wakati Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Mhe.Daniel Chongolo kwa kushirikiana na asas ya Human releif foundation walipozuru katika kituo cha watoto yatima cha Kijiji cha Furaha kilichopo Mbweni na kutoa msaada wa sukari, unga, mafuta ya kupikia na mchele kwa kituo hicho. Amesema ni jukumu letu kuhakikisha watoto hawa wanapatiwa upendo unaostahili ikiwemo haki za kisheria za watoto ambazo ni kulindwa, kusikilizwa, kupatiwa elimu, makazi na malazi. Amesema "Watoto hawa ni jukumu letu sote, lazima tuwapende na kuwajali, kwani jamii yetu imezungukwa na watu mbalimbali wanaohitaji kutazamwa kwa jicho la tatu kama vile watoto yatima na wengineo, hivyo ni wajibu wetu kuwapatia vitu wanavyohitaji".Mhe. Chongolo Ameongeza kuwa kilichofanywa leo na Mr Mbarak F.Baghumesh kutoka asas ya Human Releif Foundation ni ishara kubwa ya upendo na inatakiwa kuigwa na kila mtu, kwani hata yeye hajaangalia dini yake isipokuwa ametanguliza upendo na uthamani wa kiutu. Aidha ameahidi kushirikiana bega kwa bega na wadau wengine katika kuhakikisha changamoto mbalimbali zinazoikabiri taasisi ya Kijji cha Furaha zinatatuliwa na kuwataka watu wa idara ya ustawi wa jamii Manispaa ya Kinondoni kutafuta njia mbadala za kuwasaidia watoto yatima wanaomaliza shule katika vituo mbalimbali. Kwa upande wake Mr Mbarak ambaye ni Operation Manager wa shirika la Human Relief Foundation, amesema kuwa mbali na kutoa msaada hui, ataendelea kushirikiana na ofisi ya Mkuu wa Wilaya katika kuwathamini watu wenye mahitaji maalum bila kujali rangi wala dini zao. Imeandaliwa na Kitengo Cha Habari na Uhusiano Manispaa ya Kinondoni. WADAU NA JAMII KWA UJUMLA WAMETAKIWA KUONESHA UPENDO KWA KUWAKUMBUKA NA KUWAJALI WATU WENYE UHITAJI MAALUMU KATIKA JAMII. Posted On: May ... + Read more »
DC KINONDONI AKEMEA VIKALI WAKANDARASI WAZEMBE Posted On: May 31st, 2019 NI WALE WASIOFANYA KAZI ZAO KWA WELEDI, HALI INAYOPELEKEA UCHELEWESHWAJI WA UKAMILISHAJI WA MIRADI YA MAENDELEO. Kauli hiyo imetolewa leo, na Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Mhe Daniel Chongolo katika ziara yake ya ukaguzi wa utekelezaji wa miradi ya maendeleo ili kujiridhisha na hatua za utekelezaji zilizofikiwa. Amesema wakandarasi ni lazima waelewe umuhimu wa kutekeleza na kukamilisha miradi hii kwa mujibu wa makubaliano na mikataba waliyoingia kwani kwa kutokufanya hivyo kunarudisha nyuma maendeleo na ni kutoitendea haki si tu Serikali bali hata wananchi walengwa wa mradi unaotekelezwa. Aidha Mhe. Chongolo ameonesha kutoridhishwa na kasi ya ujenzi wa kiwanda cha kuchakata taka kinachojengwa na mkandarasi wa Kampuni ya CRJE East Africa LTD kwani katika kipindi Cha miezi 11 ya mkataba wake mradi huo umekamilika kwa asilimia 20 pekee na huku akiwa amebakiwa na miezi 7 ya kumaliza mkataba. Amesema "wakandarasi Kama hao hawatavumiliwa katika Wilaya yangu na endapo itafika tarehe 30 mwezi June bila kuonesha dalili za mabadiliko ya mradi huo mkandarasi huyu achukuliwe hatua sitahiki.", Mh. Chongolo. Kadhalika amekemea tabia ya baadhi ya wakandarasi wakubwa kuchukua tenda za Ujenzi na baadae kuwapa kandarasi wengine au wadogo kuifanya kazi hiyo, huku wao wakibaki kuwa kama madalali. Katika hatua nyingine amewataka watendaji wa Kata kusimamia kwa ukaribu miradi hiyo ili iweze kukamilika kwa wakati na iweze kuleta tija kwa jamii Miradi iliyotembelewa na Mkuu wa wilaya leo ni pamoja na Barabara ya Tegeta nyuki, Barabara ya Boko Magereza, Hospitali ya Wilaya ya Mabwepande, Shule ya wasichana ya Mabwe Tumaini girls, Kiwanda cha kuchakata taka kilichopo Mabwepande na Shule ya wavulana ya Mbweni Teta. Imeandaliwa na Kitengo Cha Habari na Uhusiano Manispaa ya Kinondoni. DC KINONDONI AKEMEA VIKALI WAKANDARASI WAZEMBE Posted On: May 31st, 2019 NI WALE WASIOFANYA KAZI ZAO KWA WELEDI, HALI INAYOPELEKEA UCHE... + Read more »