DC CHONGOLO AKABIDHI MADARASA, OFISI ZA WALIMU KATIKA SHULE YA SEKONDARI TWIGA NA KIGOGO ,AMPONGEZA MKURUGENZI Posted On: November 26th, 2019 Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Mhe. Daniel Chongolo amekabidhi madarasa sita na ofisi tatu za walimu katika Shule ya Sekondari Kigogo iliyopo Kata ya Kigogo na Shule ya Sekondari Twiga iliyopo Kata ya Wazo ikiwa ni sehemu ya mkakati wake wa kujenga vyumba 100 vya madarasa ili kuondoa tatizo la wanafunzi wanaomaliza darasa la saba kukosa nafasi ya kwenda shule kwa changamoto ya upungufu wa madarasa. Akizungumza katika uzinduzi huo, Mhe. Chongolo amesema ujenzi huo unaendelea kwa juhudi zake binafsi kwa kushirikiana na wadau mbalimbali wapenda maendeleo katika wilaya yake, hivyo anawashukuru wadau hao walioshirikiana naye kwani kukamilika kwa madarasa hayo kutasaidia wanafunzi wote wanaomaliza darasa la saba kuendelea na masomo ya Sekondari badala ya kukaa nyumba. Amesema kuwa Serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Rais Dk. John Magufuli iliamua kutoa elimu bure kwa kila mmoja ili kuhakikisha kwamba hakuna mtoto anayekaa nyumbani bila kusoma na kwamba atahakikisha madarasa hayo yanakamilishwa ili kutimiza adhma hiyo. Amefafanua kuwa kutokana na mpango wa elimu bure uliotolewa na Rais Dk. Magufuli kumekuwa na ongezeko kubwa la watoto wanaoandikishwa shule hivyo serikali itahakikisha kila mmoja anapata nafasi ya kusoma wakiwa kwenye vyumba vya madarasa. “ Awali tulikuwa na changamoto ya walimu lakini Mhe. Rais amehakikisha kuwa changamoto hiyo imekwisha ,hivi sasa tunachangamoto ya vyumba vya madarasa , hili nalo litakwisha, niwahakikishie serikali ya awamu ya tano ipo pamoja na wananchi wake” amesema Mhe. Chongolo. Nakuongeza kuwa” leo hii nimekuja mwenyewe kuzindua madarasa haya ili kuona ufanisi uliopo, niseme tu kwamba nimeridhishwa na nimefurahi kuona madarasa haya yamekamilika, sasa imebaki viti na meza ili wanafunzi waweze kusoma na nimeambiwa tayari vimeshaagizwa. Aidha amempongeza Mkurugenzi wa Manispaa ya Kinondoni Ndugu Aron Kagurumjuli kwa kuwa begakwabega na yeye katika kusimamia na kuhakikisha lengo la ujenzi wa vyumba 100 vya madarasa kwenye Halmashauri yake linatimia. Katika hatua nyingine Mhe. Chongolo amewataka wanafunzi kusoma kwa bidii ili waweze kutimiza ndoto zao kwani viongozi wamekuwa wakifanya jitihada za kutosha kuhakikisha kwamba wanapata madarasa ya kusomea. Imetolewa na Kitengo cha Habari na Uhusiano Manispaa ya Kinondoni. DC CHONGOLO AKABIDHI MADARASA, OFISI ZA WALIMU KATIKA SHULE YA SEKONDARI TWIGA NA KIGOGO ,AMPONGEZA MKURUGENZI Posted On: November 26th, ... + Read more »
DC CHONGOLO AMUAGIZA KAMANDA WA TAKUKURU KINONDONI KUMKAMATA NA KUMCHUNGUZA MKANDARASI ANAYEDAIWA KUIBA MILIONI 54 ZA WANANCHI Posted On: November 22nd, 2019 Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Mhe. Daniel Chongolo amemuagiza Kamanda wa Takukuru Mkoa maalumu wa Kinondoni kumchunguza Mkandarasi wa Savei anayesimamia urasimishaji makazi ya wananchi kanda ya Madale two , David Emanuel kutokana na tuhuma ya kudaiwa kuiba kiasi cha shilingi milioni 52 fedha zilizochangwa na wananchi. Ameongeza kuwa milioni 52 zimelipwa pasipokufuata utaratibu kutokana na mkandarasi huyo kuwa sehemu ya waweka saini katika akaunti ya wananchi na kwamba alichokuwa anakifanya nikwenda mwenyewe benki na kuchukua fedha.. Mhe. Chongolo amefikia uamuzi huo leo katika kikao chake na Kamati zilizoundwa na wananchi kwa ajili ya kuratibu na kusimamia zoezi la urasimishaji pamoja na wakandarasi waliopewa jukumu la urasimishaji makazi ya wananchi katika Halmashauri hiyo . Mhe. Chongolo ameeleza kuwa mkandarasi huyo alijilipa mwenyewe fedha hizo pasipokufuata utaratibu na kwamba kitendo hicho ni matumizi mabaya ya fedha za wananchi na kuagiza Takukuru Kinondoni kumchukulia hatua pindi atakapobainika ukweli dhidi ya tuhuma hizo. Amefafanua kuwa katika kanda hiyo, viwanja zaidi ya 1800 vimerasimishwa na hivyo wananchi wamechanga kiasi cha shilingi zaidi ya milioni 70 na kwamba hadi sasa mkandarasi huyo ameshalipwa shilingi milioni 62 ambapo kati ya hizo milioni 12 ndio zilizolipwa kwa kufuata utaratibu. “ Sasa ukiona hivi unajua kabisa kunachangamoto ya matumizi yasio yasihi ya fedha za wananchi,nimechukua hatua nimemkabidhi Kamanda wa Takukuru mkoa maalumu wa Kinondoni, wamemchukua wanakwenda kushugulikia kufanya uchunguzi na pale watakapobaini kunaukiukwaji watamchukulia hatua” amesema Mhe. Chongolo. Nakuongeza kuwa” kulingana na changamoto ambayo tumeibaini leo kwenye mtaa mmoja, nimeagiza kitengo cha ukaguzi wa ndani kwenda kukagua akaunti zote za urasimishaji ndani ya Halmashauri yetu ,ili kujiridhisha na yale watakayo yabaini sisi watuletee ripoti ilituweze kuchukua hatua stahiki kwa wakati muafaka”. Awali Mhe. Chongolo amesema kuwa katika mkutano huo wanapokea taarifa ya kila mkandarasi juu ya mwenendo na matumizi ya fedha zinazochangwa kutoka kwa wananchi ilikukamilisha zoezi husika la urasimishaji. Amebainisha kuwa , katika mkutano huo amejifunza kuwepo na changamoto ya usimamizi wafedha za wananchi katika maeneo mengi yanayoendesha zoezi hilo ipo haja ya haraka katika kutatua changamoto hizo. Imetolewa na Kitengo Cha habari na Uhusiano Manispaa ya Kinondoni. DC CHONGOLO AMUAGIZA KAMANDA WA TAKUKURU KINONDONI KUMKAMATA NA KUMCHUNGUZA MKANDARASI ANAYEDAIWA KUIBA MILIONI 54 ZA WANANCHI Posted On:... + Read more »
ALAT YAIPONGEZA MANISPAA YA KINONDONI KWA KUTEKELEZA MIRADI MIKUBWA KWA KUTUMIA FORCE ACCOUNT, YATAKA HALMASHAURI NYINGINE ZIIGE Posted On: November 21st, 2019 Jumuiya ya Serikali za Mitaa Tanzania ( ALAT) imeipongeza Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni kwa kutekeleza miradi mikubwa ya kimkakati kwakutumia Local Fundi (Force Account). Akizungumza na watendaji wa Halmashauri hiyo mara baada ya kukamilisha ziara ya kukagua miradi ya Halmashauri hiyo, Makamu Mwenyekiti wa ALAT , Stephano Mhapa amesema kuwa Mkurugenzi Mtendaji Aron Kagurumjuli na timu yake wamefanikisha kujenga miradi mikubwa ya maendeleo kwa kutumia mafundi wa kawaida jambo ambalo limeonyesha nizamu ya matumizi mazuri ya fedha za serikali. Amefafanua kuwa mradi wa Zahanati ya Mikoroshini iliyopo Kata ya Msasani imejengwa kwa shilingi milioni 400.8 kwa kutumia mafundi wa kawaida wakati kwa mkandarasi wakutangaza tenda ingetumia milioni 700 na kwamba Halmashauri hiyo imeokoa kiasi cha shilingi milioni 300. Aidha Mhapa amesema kuwa“ ukiangalia Zahanati hii imekamilika vizuri na imara , tumejionea wenyewe, Mkurugenzi na timu yako tunakupongeza sana, na halmashauri nyingine ziige mfano huu kutoka kwako, kazi ni kubwa uliyoifanya lakini gharama yake ni ndogo, haya ni matumizi mazuri ya fedha za serikali.” Akizungumzia mradi wa Soko la kisasa la Magomeni, linalojengwa kwa shilingi zaidi ya bilioni 8.9 na Kituo cha Afya kilichopo Kigogo kinachojengwa kwa shilingi milioni 700 , Mhapa amesisitiza kuwa Halmashauri ya Kinondoni inapaswa kuigwa na Halmashauri nyingine kwa kazi kubwa wanayoifanya sambamba na kuwa na matumizi mazuri ya serikali. “ Halmashauri ya Kinondoni tangu mwaka 2015 imekuwa ikipata hati safi na hiyo ni kutokana na kuwa na nidhamu ya matumizi mazuri ya fedha za serikali, hati safi inamanisha kwamba mnapokea pesa za serikali lakini pia mnakusanya mapato ya ndani na kuyatumia vizuri” ameongeza. Kuhusu asilimia 10 ya fedha kwa ajili ya mikopo ya vijana , wakina mama na walemavu,ambayo ni bilioni tatu, Katibu wa ALAT Elirehema Kaaya ameipongeza Halmashauri kwakufanya vizuri kwani kiasi hicho cha fedha ni sawa na bajeti nzima ya Halmashauri nyingine. Kaaya amesisistiza kuwa kazi anayoifanya Mkurugenzi Kagurumjuli ndio inayotakiwa na Rais Dk. John Magufuli na hivyo kuagiza Halmashauri nyingine ziige mfano wake. “ Umefanya matumizi mazuri na sahihi ya fedha ambazo ni kodi za wananchi wanyonge, kilichofanyika na Mkurugenzi mtedaji wa Kinondoni ni kwamba , Mhe. Rais Magufuli na Waziri wa Tamisemi Suleman Jafo wanasisitiza kutumia local fundi (Force Account) ninashauri wakurugenzi wengine wasikilize maagizo yanatotolewa na serikali.” Amesisitiza Kaaya. Awali akizungumza na viongozi wa ALAT, Mkurugenzi wa Manispaa ya Kinondoni Ndg Aron Kagurumjuli amesema kuwa Halmashauri imefanikiwa kupata bilioni 32.8 kutoka Serikali kuu kwa ajili ya ujenzi wa miradi mitatu ya kimkakati ambayo itaongeza mapato kwa kiasi kikubwa. Kagurumjuli alitaja miradi hiyo kuwa ni ujenzi wa soko la kisasa la Magomeni, wenye thamani ya shilingi bilioni 8.9, ujenzi wa soko la kisasa la Tandale wenye thamani ya shilingi bilioni 8.7 na uboreshaji wa fukwe ya Osterbay (Coco Beach) wenye gharama ya shilingi bilioni 13. Imeandaliwa na Kitengo cha Habari na Uhusiano Manispaa ya Kinondoni ALAT YAIPONGEZA MANISPAA YA KINONDONI KWA KUTEKELEZA MIRADI MIKUBWA KWA KUTUMIA FORCE ACCOUNT, YATAKA HALMASHAURI NYINGINE ZIIGE Posted O... + Read more »
DC CHONGOLO AWAWEKA NDANI WAKANDARASI WA KAMPUNI YA CRJE KWA KUSHINDWA KUKAMILISHA MRADI WA KUCHAKATA TAKA KWA WAKATI Posted On: November 19th, 2019 Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni , Mhe. Daniel Chongolo amewashikilia wakandarasi wawili wenye asili ya china wa Kampuni ya CRJE kwa kushindwa kukamilisha mradi wa ujenzi wa kiwanda cha kuchakata taka kilichopo Mabwepande. Mhe. Chongolo amefikia uamuzi huo leo mara baada ya kampuni hiyo kushindwa kukamilisha mradi huo kwa wakati huku Mhandisi mshauri wa Manispaa Emanuel Tilya akisisitiza kuwa wamekuwa hawatoi ushirikiano wowote licha ya kwamba yupo kwenye eneo la mradi. Akizungumza wakati wa ziara aliyoifanya leo ya kukagua miradi inayojengwa na Halmashauri hiyo, Mhe. Chongolo amefafanua kuwa kwa muda mrefu amekuwa akizungumza na mkandarasi huyo kuhusu kukamilisha mradi huo kwa muda uliopangwa lakini hawakufanya hivyo . Ameeleza kuwa halmashauri inahitaji kiwanda hicho haraka ili kiweze kutumiwa na wananchi ambao ndio wanufaika wa mradi huo lakini mkandarasi aliyepewa kazi hiyo anawarudisha nyuma. Ameeleza kuwa halmashauri imeshawalipa fedha kwa ajili ya ujenzi huo lakini kinachofanyika ni fedha hizo kuzipeleka kwenye miradi yao mingine jambo ambalo limefanya hadi sasa kusuasua kwa mradi. “ Nimekuja hapa zaidi ya mara tatu, mara ya kwanza nilikuja nikaongea nao wakaniahidi watakamilisha kwa muda uliopangwa, mara ya pili nilikuja hapa nikafoka hadi nikakasirika lakini hali imeendelea hivi hivi, sasa sijawakamata nimewashikilia hadi pale watakapoleta mpango kazi wao uliojitosheleza.“ amesema Mhe. DC. ”Hatuwezi kukaa na watu wa namna hii, tumetoa pesa nyingi, kwa ajili ya kukamilisha mradi huu mapema halafu wanatuchezea, ,kama wakileta leo, kesho nitawaachia, kadiri watakavyowahi kuniletea huo mpango kazi wao ndio na mimi nitawaachia, Askari kamata hao waweke ndani. Mhe. Chongolo alisisitiza kuwa hajaridhishwa na mwenendo wa ujenzi wa kiwanda hicho na kuagiza wasiachiwe hadi atakapotoa agizo ikiwa ni baada ya kutekeleza walichoambiwa. Awali Mhandisi mshauri wa Manispaa, mhandisi Tilya ,amesema kuwa walikubaliana kufanya kazi usiku na mchana ili kukamilisha ujenzi huo kwa wakati lakini kilichotokea ni tofauti huku mafundi wanne tu ndio waliokuwa wanafika eneo hilo la mradi. Alifafanua kuwa “ wakati mwingine huwa tunagombana wenyewe kwa wenyewe, kama angekuwa na uwezo wakufanya kazi kama msambazaji wake ingekuwa sawa, kwani anauwezo wakubeba kiubiki mita. 150 hadi kufikia saa 8.00 mchana, inamana tukifanya kazi usiku na mchana tunaweza kufikia kiubiki mita .300 kwa siku. Alifafanua kuwa eneo la kiwanda hicho kinaukubwa wa mita zaidi ya 4070 ambapo hadi sasa tayari imeshafanyika kiubiki mita 491 sawa na asilimia 12 na kwamba iliaweze kufanikisha hanabudi ndani ya mwezi mmoja kwa usiku na mchana jambo ambalo alisema mkandarasi huyo hawezi kufanya. Mhandisi huyo alifika mbali zaidi nakusema kuwa “ hakuna ushirikiano ambao anapata kutoka kwao , wanachoendelea kukifanya hapa ni kukudanganya mkuu. Imetolewa na Kitengo cha Habari na Uhusiano Manispaa ya Kinondoni. DC CHONGOLO AWAWEKA NDANI WAKANDARASI WA KAMPUNI YA CRJE KWA KUSHINDWA KUKAMILISHA MRADI WA KUCHAKATA TAKA KWA WAKATI Posted On: November... + Read more »
DC CHONGOLO ATAKA USAWA KWA WATU WENYE ULEMAVU, ASEMA WASINYANYAPALIWE Posted On: November 15th, 2019 Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Mhe. Daniel Chongolo ameiasa jamii kutojihusisha na tabia ya kuwanyanyapaa watu wenye ulemavu kwakuwa na wao wana haki ya kupata haki zote kama ilivyo kwa watu wengine. Mhe. Chongolo ametoa kauli hiyo leo wakati wa uzinduzi wa kamati ya watu wenye ulemavu uliofanyika Manispaa ya Kinondoni ambapo pamoja na mambo mengine amesema ipo dhana iliyojengeka ya kuwanyanyapaa watu hao na hivyo kueleza kuwa kufanya hivyo ni makosa na kusisitiza kuwa nilazima itendeke haki na usawa. Amesisitiza kuwa watu wenye ulemavu wanahaki ya kupewa nafasi mbalimbali na kusema kuwa wote wenye dhamana ya uongozi katika Halmashauri hiyo ni lazima kuangalia makundi hayo kwa upekee zaidi kwa kutenda haki na usawa. Mhe. Chongolo amefafanua kuwa ili kufikia malengo hayo kila mmoja hakuna budi kushirikiana na kamati hiyo iliyoundwa kuweka miundombinu sawia itakayowezesha walemavu kuishi kwa kupata haki zao na usawa pamoja na kuepusha kunyanyapaliwa kama ilivyo kwa sasa. “ Nawashukuru sana kwakunipa heshima hii ya kuzindua kamati hii ambayo inalenga kusimamia, kushughulikia ipasavyo kutetea haki na usawa wawatu wenye ulemavu” amesema Mhe. Chongolo. Mhe. Chongolo hakusita kueleza changamoto mbalimbali zilizopo katika Halmashauri ya Kinondoni na kusema kuwa sio vijijini tu hata mijini wapo baadhi ya watu wanao wanyanyapaa walemavu kwakuwatenga, kuwaficha pamoja na kuwanyima fursa yakupatiwa huduma kama watu wengine. “ Jamii imekuwa na taswira mbaya yakuona kwamba ulemavu ni changamoto iliyokuwa na madhara , na hivyo kujikita kunyanyapaa, kamati hii imepewa mamlaka, sasa nendeni mkajenge timu nzuri itakayoleta sura ya kubadilisha mtazamo uliopo hivi sasa na kuleta matunda na faida kwao. Awali taarifa ya watu wenye ulemavu, ilieleza kuwa halmashauri inajumla ya kata 20 ambazo zinahudumia watu hao wapatao 1239 ambapo kati yao wanaume ni 724 na wanawake 515. Aidha taarifa hiyo ilieleza kuwa kati ya watu hao wakubwa ni 973 huku watoto wakiwa 266 na kwamba huduma hizo zinatolewa kwakuzingatia sera ya watu wenye ulemavu ya mwaka 2004, sheria namba 9 ya mwaka 2010 pamoja na mikataba mbalimbali inayohusu watu wenye ulemavu. Ameeleza kuwa , Halmashauri imekuwa ikiviwezesha vyama vya watu wenye ulemavu kwa kuvipatia vifaa saidizi kulingana na aina ya ulemavu sambamba na kuwapatia misaada au kujikimu kwa walio na mazingira hatarishi. Aidha ameeleza kuwa , Kinondoni imekuwa ikiwaunganisha na asasi za kiraia ili waweze kujipatia ujuzi , ajira na misaada ya kujikumu palipo na uhitaji pamoja na kuwawezesha maadhimisho ya watu wenye ulemavu yanayofanyika kila mwaka. Imeandaliwa na Kitengo cha Habari na Uhusiano Manispaa ya Kinondoni. DC CHONGOLO ATAKA USAWA KWA WATU WENYE ULEMAVU, ASEMA WASINYANYAPALIWE Posted On: November 15th, 2019 Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Mhe.... + Read more »
MEYA SITA ASHAURI WANANCHI KUPENDA BIDHAA ZINAZO ZALISHWA NCHINI, ASEMA ZINA UBORA WA HALI YA JUU Posted On: November 15th, 2019 Mstahiki Meya wa Manispaa ya kinondoni, Mhe. Benjamini Sita ametoa kauli hiyo leo alipokuwa akikagua mabanda ya maonesho ya wajasiriamali yaliyoandaliwa na Manispaa ya Kinondoni na kuwezeshwa na Mamlaka ya Biashara Tanzania Tan Tredi. Amesema upo mtazamo kwa wananchi waliowengi kuwa bidhaa zinazozalishwa nchini hazina ubora, lakini zipo bidhaa za ngozi zinazozalishwa nchini zenye ubora hivyo amefurahishwa na Manispaa kuandaa maonesho hayo kwani kufanya hivyo ni njia mojawapo ya kuwatia moyo wajasiriamali na hivyo kupata fursa ya kutangaza bidhaa zao. "Tanzania inauwezo mkubwa wa kuzalisha bidhaa za ngozi zenye ubora kutoka kwa wajasiriamali wa ndani na hivyo wananchi waondoe dhana ya watu kwenda kununua bidhaa hizo nje ya nchi" Amesisitiza Mstahiki Meya Kwaupande wake Mkuu wa Idara ya Mifugo na Uvuvi,Dk. Patricia Henjewele alisema kuwa maonesho hayo yamekwenda sambamba na mafunzo ya utangazaji wa bidhaa ambapo wajasiriamali kutoka Manispaa ya Kinondoni wameshiriki na baada ya kumalizika kwa mafunzo na maonesho hayo, Halmashauri imeandaa maonesho mengine yatakayofanyika Disemba 12 hadi 15 katika viwanja vya Tanganyika Pekazi ambapo wajasiriamali kutoka sehemu mbalimbali watashiriki. Kwa upande wao washiriki wa maonesho hayo wameipongeza manispaa ya Kinondoni kwakuandaa mafunzo hayo kwani imekuwa fursa kutangaza bidhaa ambazo wamezizalisha wenyewe na hivyo kuomba wananchi kuwaunga mkono. Imetolewa na Kitengo cha habari na uhusiano Manispaa ya Kinondoni. MEYA SITA ASHAURI WANANCHI KUPENDA BIDHAA ZINAZO ZALISHWA NCHINI, ASEMA ZINA UBORA WA HALI YA JUU Posted On: November 15th, 2019 Mstahi... + Read more »
DC CHONGOLO AWAFUNDA VIJANA WAJASIRIAMALI WA BIDHAA ZA NGOZI KUCHANGAMKIA FURSA ZA MIKOPO YA HALMASHAURI Posted On: November 14th, 2019 Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Mhe. Daniel Chongolo amewataka vijana kutumia fursa inayotolewa na serikali kupitia halmashauri kupata mikopo isiyokuwa na riba ili waweze kujikwamua kiuchumi. Mhe. Chongolo alitoa kauli hiyo jana wakati akifungua mafunzo kwa vijana wajasiriamali wanaotengeneza bidhaa za ngozi waliopo katika Manispaa ya Kinondoni ambapo miongoni mwao walipata fursa ya kushiriki maonesho ya wakulima nanenane. Mhe. Chongolo alisema kuwa Manispaa ya Kinondoni inafungu la bajeti kwa ajili ya kutoa mikopo kwa Vijana, wakina mama na watu wenye ulemavu kwa lengo la kuwasaidia kujikwamua katika umasikini hivyo vijana wanapaswa kutumia nafasi hizo wanazozipata kwani itawawezesha kukuza mitaji yao na hivyo kufikia lengo la kuwa na viwanda huku akitolea mfano wa mfanyabiashara mkubwa Marehemu Dk. Reginal Mengi ambaye alifanikiwa kuwa na viwanda kupitia ujasiriamali. Alifafanua kuwa iwapo watatumia vizuri mafunzo hayo yataleta tija katika kukuza uchumi wa ndani na kwamba serikali kupitia halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni itasimamia kupata mikopo hiyo na hivyo kuwawezesha kupata mashine pamoja na eneo la kujenga kiwanda chakutengeneza bidhaa za ngozi. “ Nawapongeza sana idara husika ambayo imeandaa haya mafunzo sambamba na maonyesho ya bidhaa za ngozi, vijana mliopo hapa ,tumieni hii fursa mliyoipata, hakuna mafanikio ya siku moja, wote waliofanikiwa walianza kama nyie hapa” alisema Mhe. Chongolo. “ Tunahitaji watu ambao watakuwa na nia ya kweli ya kujikwamua kiuchumi, inawezekana kuzalisha bidhaa za ngozi kwakuwa Tanzania tunaongoza kwakuwa na mifugo, ukiangalia Dar es Salaam ndio inaongoza kwa kula nyama,kwahiyo tunazana za kutengenezea bidhaa zetu” alifafanua. Kwaupande wake , Meneja ukuzaji Bidhaa kutoka Tan Tredi , Masha Husein alisema kuwa wataendelea kushirikiana na manispaa ya Kinondoni katika kuwaelimisha wajasiriamali namna ya kufanya biashara kwenye maonesho kwani hiyo imekuwa ni changamoto kubwa kwao. Alifafanua kuwa, wajasiriamali wengi hawana uelewa wa kutosha kuhusiana na namna ya kushiriki kwenye maonesho mbalimbali wanapopata nafasi jambo ambalo kama Tan Tredi imeliona na hivyo kusisitiza kuwa watahakikisha wanatoa elimu hiyo ili waweze kunufaika. Naye Mkuu wa Idara ya Mifugo na Uvuvi Dk. Patricia Henjewele alimpongeza Mhe. Chongolo kwakujali vijana na kusema kuwa katika maonesho ya nane nane waliona umuhimu wakukutana na wajasiriamali hao na hivyo kuandaa semina hiyo iliyoambatana na maonesho. Aidha aliwapongeza Tan Tredi kwakuwezesha maonesho hayo na hivyo kuahidi kuendeleza ushirikiano zaidi katika kutoa elimu kwa wajasiriamali hao. Imetolewa na Kitengo cha Habari na Uhusiano Manispaa ya Kinondoni. DC CHONGOLO AWAFUNDA VIJANA WAJASIRIAMALI WA BIDHAA ZA NGOZI KUCHANGAMKIA FURSA ZA MIKOPO YA HALMASHAURI Posted On: November 14th, 2019 ... + Read more »