Top ad

Top ad

 

MAENDELEO YA JAMII KINONDONI WATEMBELEA ENEO LA VIWANDA VIDOGO SIDO

Posted On: February 11th, 2021

Maafisa maendeleo ya jamii 25 kutoka Manispaa ya Kinondoni kwa kushirikiana na Taasisi isiyo ya Kiserikali PAKACHA  wamefanya ziara kutembelea eneo la viwanda vidogo SIDO Vingunguti kwa lengo la kujionea  mashine mbalimbli zinazozalishwa na SIDO ambapo Manispaa inaweza kukopesha kupitia mfumo ya kuwezesha Wananchi kiuchumi.

Akiongea wakati wa ziara hiyo, mratibu wa mradi kutoka Taasisi ya Pakacha Bw. Haruni Jongo amesema wameamua kuwezesha ziara hiyo kwa sekta hiyo kwani wanaamini kwamba wakipata uelewa  mpana juu ya bidhaa zinazopatikana hapa nchini watakuwa mabalozi wazuri kwa wanufaika mikopo

Naye Mkuu wa Idara ya Maendeleo ya Jamii Bi Halima kahema alipokuwa akizungumza  ameishukuru Taasisi ya pakacha kwa kuwezesha Maafisa kutembelea SIDO, kwani wamekutana na teknolojia mpya ambazo wajasiriamali wanaweza kutumia na kuleta tija katika uzalishaji wa bidhaa zao.

 Amesema  kwa kutoa mikopo ya vitendea kazi itasaidia wanufaika hao kutumia mikopo yao kwa Lengo husika na kuwataka Maafisa Maendeleo kutumia uelewa walioupata kiwandani hapo kuwahamasisha vijana, walemavu na wanawake wanaotaka mikopo ya  kununua vifaa kuwapa elimu sahihi ya vifaa na mahali vinapopatikana.

Kinondoni kwa mwaka wa fedha unaoisha Ilitenga kiasi cha   Tsh Bil 3.4 kwaajili ya mikopo ya vijana, wanawake na walemavu ambapo vikundi mbalimbali vinaendelea kunufaika na mikopo hiyo.


Imeandaliwa na

Kitengo cha Habari na Uhusiano

Manispaa ya Kinondoni.

0 comments:

Post a Comment

 
Top