UWASILISHWAJI WA TAARIFA ZA KAMATI ZA KUDUMU-BARAZA LA MADIWANI.Posted On: March 17th, 2021Mhe Michael Urio, Diwani wa Kata ya Kunduchi na Mwenyekiti wa Kamati ya kudumu ya Huduma za Uchumi,Afya na elimu akiwasilisha taarifa ya utendaji kazi wa kamati hiyo robo ya pili.Wenyeviti wa kamati tano za kudumu waliwasilisha taarifa zao katika mkutano huo. Kamati hizo ni Kamati ya Huduma za Uchumi afya na elimu, Kamati ya Maadili, Kamati ya fedha na Uongozi, Kamati ya kudhibiti UKIMWI na Kamati ya Mipangomiji.Imeandaliwa na Kitengo cha Habari na UhusianoManispaa ya KinondoniMatangazoTANGAZO KUHUSU VIBANDA VYA MWENGEFebruary 22, 2021TAARIFA KUHUSIANA NA WASTAAFU WANAOLIPWA NA HAZINAFebruary 18, 2021TANGAZO KUHUSU WAMILIKI WA KUMBI ZA BURUDANI, SHEREHE NA BAAJanuary 22, 2021HAWA HAPA WADAIWA SUGU WA LESENI ZA BIASHARA MANISPAA YA KINONDONIDecember 04, 2020Tazama zoteHabari mpyaMSTAHIKI MEYA MANISPAA YA KINONDONI MHE. SONGORO MNYONGE AKIFAFANUA JAMBO WAKATI WA BARAZA LA MADIWANIMarch 17, 2021 UWASILISHWAJI WA TAARIFA ZA KAMATI ZA KUDUMU-BARAZA LA MADIWANI.March 17, 2021 MKURUGENZI WA MAISPAA BI SIPORA LIANA AKITOA UFAFANUZI WA JAMBO WAKATI WA BARAZA LA MADIWANI.March 17, 2021 HABARI KATIKA PICHA-MKUTANO WA BARAZA LA MADIWANI.March 17, 2021Tazama zote UWASILISHWAJI WA TAARIFA ZA KAMATI ZA KUDUMU-BARAZA LA MADIWANI. Posted On: March 17th, 2021 Mhe Michael Urio, Diwani wa Kata ya Kunduch... + Read more »
MKURUGENZI WA MAISPAA BI SIPORA LIANA AKITOA UFAFANUZI WA JAMBO WAKATI WA BARAZA LA MADIWANI.Posted On: March 17th, 2021Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni Bi Sipora Liana akitoa majibu na ufafanuzi wa maswali ya papo kwa papo katika Mkutano wa Baraza la Madiwani la kupitisha Taarifa ya mapato na matumizi robo ya pili 2020/2021.Jumla ya maswali matano ya papo kwa papo yaliulizwa na kutolewa majibu na ufafanuzi kuhusu sekta za elimu, miundombinu na ustawi wa Manispaa kwa ujumla.Imeandaliwa naKitengo cha Habari na UhusianoManispaa ya Kinondoni.MatangazoTANGAZO KUHUSU VIBANDA VYA MWENGEFebruary 22, 2021TAARIFA KUHUSIANA NA WASTAAFU WANAOLIPWA NA HAZINAFebruary 18, 2021TANGAZO KUHUSU WAMILIKI WA KUMBI ZA BURUDANI, SHEREHE NA BAAJanuary 22, 2021HAWA HAPA WADAIWA SUGU WA LESENI ZA BIASHARA MANISPAA YA KINONDONIDecember 04, 2020Tazama zoteHabari mpyaMSTAHIKI MEYA MANISPAA YA KINONDONI MHE. SONGORO MNYONGE AKIFAFANUA JAMBO WAKATI WA BARAZA LA MADIWANIMarch 17, 2021 UWASILISHWAJI WA TAARIFA ZA KAMATI ZA KUDUMU-BARAZA LA MADIWANI.March 17, 2021 MKURUGENZI WA MAISPAA BI SIPORA LIANA AKITOA UFAFANUZI WA JAMBO WAKATI WA BARAZA LA MADIWANI.March 17, 2021 HABARI KATIKA PICHA-MKUTANO WA BARAZA LA MADIWANI.March 17, 2021Tazama zote MKURUGENZI WA MAISPAA BI SIPORA LIANA AKITOA UFAFANUZI WA JAMBO WAKATI WA BARAZA LA MADIWANI. Posted On: March 17th, 2021 Mkurugenzi wa Ha... + Read more »
HABARI KATIKA PICHA-MKUTANO WA BARAZA LA MADIWANI.Posted On: March 17th, 2021Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni wakiwa katika mkutano wa kupitisha taarifa ya mapato na matumizi robo ya pili ya mwaka wa fedha 2020/2021. Katika kipindi hiki cha Oktoba –Desemba Halmashauri imepokea na kukusanya Jumla ya Tsh 4,938,023,120.85 sawa na asilimia 64.7% ya makisio ya kukusanya Tshs 7,629,852,875,00.Imeandaliwa naKitengo cha Habari na UhusianoManispa ya Kinondoni.MatangazoTANGAZO KUHUSU VIBANDA VYA MWENGEFebruary 22, 2021TAARIFA KUHUSIANA NA WASTAAFU WANAOLIPWA NA HAZINAFebruary 18, 2021TANGAZO KUHUSU WAMILIKI WA KUMBI ZA BURUDANI, SHEREHE NA BAAJanuary 22, 2021HAWA HAPA WADAIWA SUGU WA LESENI ZA BIASHARA MANISPAA YA KINONDONIDecember 04, 2020Tazama zoteHabari mpyaMSTAHIKI MEYA MANISPAA YA KINONDONI MHE. SONGORO MNYONGE AKIFAFANUA JAMBO WAKATI WA BARAZA LA MADIWANIMarch 17, 2021 UWASILISHWAJI WA TAARIFA ZA KAMATI ZA KUDUMU-BARAZA LA MADIWANI.March 17, 2021 MKURUGENZI WA MAISPAA BI SIPORA LIANA AKITOA UFAFANUZI WA JAMBO WAKATI WA BARAZA LA MADIWANI.March 17, 2021 HABARI KATIKA PICHA-MKUTANO WA BARAZA LA MADIWANI.March 17, 2021Tazama zote HABARI KATIKA PICHA-MKUTANO WA BARAZA LA MADIWANI. Posted On: March 17th, 2021 Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni ... + Read more »
MGOGORO WA ARDHI ENEO LA CHASIMBA, CHACHUI ,CHATEMBO PAMOJA NA KIWANDA CHA SARUJI CHA WAZO WAFIKIA TAMATIPosted On: March 13th, 2021Mgogoro huo wa kiwanja chenye ukubwa wa hecta 224.8 uliodumu kwa takribani Miaka Saba ukihusisha wananchi wapatao 4000 kutoka cha simba chatembo, chachui pamoja na kiwanda cha saruji cha Wazo umemalizika leo.Hatua hiyo imefikiwa baada ya Waziri wa Ardhi, nyumba na maendeleo ya makazi Mhe.William lukuvi kukutana na wananchi katika mkutano wa hadhara na kutoa mapendekezo yaliyofikiwa katika mazungumzo ya muda mrefu kati ya Serikali na bodi ya kiwanda cha saruji kuhusiana na mstakabali wa wananchi katika eneo ambalo thamani yake ni takribani bilioni 60 za kitanzania.Amesema " Leo tunabadilisha historia ya kuitwa wavamizi , na kuwa wamiliki halali baada ya kila mmoja wenu kutimiza wajibu wake unaompasa ndani ya miezi sita kuanzia Sasa, utakaompa kila mwananchi haki ya kumiliki kihalali baada ya taratibu zote za umilikishwaji kukamilika. Hii ndio Serikali ya Dr.John Pombe Joseph Magufuli inayojali wananchi wanyonge" Mhe. William Lukuvi..Aidha amesisitiza kuwa lengo la Serikali si kuingilia muhimili wa mahakama, bali ni kutafuta suluhu yenye lengo la kunufaisha pande zote mbili kwa mstakabali wa nchi yetu.Ameongeza kuwa kukamilika kwa wajibu wa kila mwananchi kutafuatiwa na taratibu za umilikishwaji wa ardhi kihalali na upatikanaji wa maeneo muhimu kama vile maeneo ya makazi, biashara, huduma za Jamii, maeneo ya shule, zahanati, ofisi chekechea, makanisa na masoko.Katika hatua nyingine Mhe. Lukuvi ameruhusu Manispaa ya Kinondoni kupeleka huduma muhimu za Jamii Kama vile shule, zahanati, vituo vya afya pamoja na kuboresha mtandao wa barabara utakaowarahisishia wananchi hao katika shughuli zao za kila siku.Mkutano huo umehudhuriwa pia na viongozi mbalimbali wakiwemo wa vyama na Serikali kwa lengo la kuongeza nguvu ya pamoja Katika kuhakikisha Sera ya Serikali ya awamu ya tano ya kutetea wanyonge inatekelezwa. Imeandaliwa naKitengo Cha Habari na Uhusiano.Manispaa ya Kinondoni. MGOGORO WA ARDHI ENEO LA CHASIMBA, CHACHUI ,CHATEMBO PAMOJA NA KIWANDA CHA SARUJI CHA WAZO WAFIKIA TAMATI Posted On: March 13th, 2021 Mgog... + Read more »
KINONDONI YAPONGEZWA KWA KUTENGA FEDHA KWA AJILI YA MIKOPO YA WANAWAKE, VIJANA NA WALEMAVUPosted On: March 9th, 2021Pongezi hizo zimetolewa leo na Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Mhe. Daniel Chongolo alipokuwa akikabidhi hundi ya kiasi cha tsh takribani Bilioni 1.3, kwa ajili ya mikopo ya wanawake, walemavu na vijana robo ya nne, fedha zilizotengwa kwa bajeti ya mwaka 2021.Amesema Kinondoni inaonesha dhamira ya dhati katika kuhakikisha inamkwamua mwanamke, kijana na mlemavu kiuchumi kwa kuwatengea fedha hizo za mikopo kwa wakati, kwa mujibu wa Sheria na kuwawezesha walengwa ."Bilioni 3.4 kwa ajili ya mikopo kwa mwaka ni fedha nyingi zilizotengwa kwa bajeti ya 2021, hivyo kinamama, vijana na watu wenye ulemavu nafasi hii ni yenu, mnapopata fedha hizo mkazitumie kwa makusudi husika na si vinginevyo." Amesema Daniel Chongolo.Akimkaribisha Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Mkurugenzi wa Manispaa hiyo Bi Sipora Liana amesema kinamama ni jeshi kubwa katika kukuza uchumi wa familia hasa kunapokuwa na fursa za mikopo na kuwahakikishia haki na usawa katika suala hilo kwani ndiyo njia pekee ya kuwawezesha mikopo yenye tija, na kufanya miradi ya maendeleo na kuwataka kurejesha fedha hizo kwa wakati ili ziweze kusaidia na wengine.Awali akitoa taarifa za mikopo na vikundi, Mkuu wa Idara ya Maendeleo ya Jamii Bi.Halima Kahema amesema hadi sasa Kinondoni imeshakopesha fedha kwa vikundi 202, vinavyohusisha wanawake , vijana na watu wenye ulemavu.Katika hatua nyingine Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Mhe.Daniel Chongolo amaewataka wanawake,vijana na walavu kuhakikisha wanarejesha fedha hizo za mikopo kwa wakati ili ziweze kusaidia na wengine, na kuwasisitiza kutumia fedha hizo kwa makusudi kamili ili waweze kufikia tija inayokusudiwa.Imeandaliwa naKitengo Cha Habari na Uhusiano.Manispaa ya Kinondoni. KINONDONI YAPONGEZWA KWA KUTENGA FEDHA KWA AJILI YA MIKOPO YA WANAWAKE, VIJANA NA WALEMAVU Posted On: March 9th, 2021 Pongezi hizo zimetol... + Read more »
MAENDELEO YA JAMII KINONDONI WATEMBELEA ENEO LA VIWANDA VIDOGO SIDOPosted On: February 11th, 2021Maafisa maendeleo ya jamii 25 kutoka Manispaa ya Kinondoni kwa kushirikiana na Taasisi isiyo ya Kiserikali PAKACHA wamefanya ziara kutembelea eneo la viwanda vidogo SIDO Vingunguti kwa lengo la kujionea mashine mbalimbli zinazozalishwa na SIDO ambapo Manispaa inaweza kukopesha kupitia mfumo ya kuwezesha Wananchi kiuchumi.Akiongea wakati wa ziara hiyo, mratibu wa mradi kutoka Taasisi ya Pakacha Bw. Haruni Jongo amesema wameamua kuwezesha ziara hiyo kwa sekta hiyo kwani wanaamini kwamba wakipata uelewa mpana juu ya bidhaa zinazopatikana hapa nchini watakuwa mabalozi wazuri kwa wanufaika mikopoNaye Mkuu wa Idara ya Maendeleo ya Jamii Bi Halima kahema alipokuwa akizungumza ameishukuru Taasisi ya pakacha kwa kuwezesha Maafisa kutembelea SIDO, kwani wamekutana na teknolojia mpya ambazo wajasiriamali wanaweza kutumia na kuleta tija katika uzalishaji wa bidhaa zao. Amesema kwa kutoa mikopo ya vitendea kazi itasaidia wanufaika hao kutumia mikopo yao kwa Lengo husika na kuwataka Maafisa Maendeleo kutumia uelewa walioupata kiwandani hapo kuwahamasisha vijana, walemavu na wanawake wanaotaka mikopo ya kununua vifaa kuwapa elimu sahihi ya vifaa na mahali vinapopatikana.Kinondoni kwa mwaka wa fedha unaoisha Ilitenga kiasi cha Tsh Bil 3.4 kwaajili ya mikopo ya vijana, wanawake na walemavu ambapo vikundi mbalimbali vinaendelea kunufaika na mikopo hiyo.Imeandaliwa naKitengo cha Habari na UhusianoManispaa ya Kinondoni. MAENDELEO YA JAMII KINONDONI WATEMBELEA ENEO LA VIWANDA VIDOGO SIDO Posted On: February 11th, 2021 Maafisa maendeleo ya jamii 25 kutoka Ma... + Read more »
BARAZA LA MADIWANI KINONDONI LAPITISHA TAARIFA YA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEOPosted On: January 7th, 2021Baraza hilo chini ya Mwenyekiti wake Mhe.Songoro Mnyonge limeipitisha taarifa hiyo ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo robo ya kwanza Julai hadi Septemba 2020/2021 katika kikao cha baraza kilichofanyika leo katika ukumbi wa mikutano wa Manispaa.Akipitisha taarifa hiyo Mhe.Songoro amesema taarifa hii ya utekelezaji ni ile ya bajeti inayomalizika miezi michache ijayo hivyo imetekelezwa kwa kiwango cha kuridhisha na kuwataka Madiwani kuorodhesha mahitaji yao katika bajeti ijayo ya 2021/2122."Mimi niwashauri Wahe.Madiwani bajeti tunayotekeleza sasa tumeikuta, imebakiza miezi michache, lakini mchakato wa kuandaa bajeti ijayo tayari umeshaanza katika ngazi ya Halmashauri, hivyo niwaombe Wahe.madiwani twende tukapitie mipango yetu ili tuiingize kwenye mpango wa bajeti" Amesema Mstahiki.Akiwasilisha taarifa hiyo ya utekelezaji katika kikao cha Baraza hilo Katibu wa kikao hiko ambaye pia ni Mkurugenzi wa Manispaa ya Kinondoni Ndg Aron Kagurumjuli amesema kwa mwaka wa fedha 2020/2021 Manispaa ilipanga kutumia jumla ya shilingi takribani Bilioni 30.5 kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo.Amesema fedha hizo zimetokana na vyanzo mbalimbali na kuvitaja kuwa ni mapato ya ndani ya Halmashauri, ruzuku kutoka Serikali kuu pamoja na nguvu ya jamii.Katika kikao hicho cha baraza Wahe.Madiwani ambao ni wenyeviti wa kamati za kudumu pia walipata fursa ya kuwasilisha taarifa za utekelezaji wa shughuli za kamati zao.Taarifa zilizowasilishwa katika baraza hilo ni za kamati za kudumu robo ya kwanza Julai hadi Septemba 2020/2021 ambazo ni taarifa za huduma za Uchumi afya na Elimu, taarifa za kamati ya mipangomiji na mazingira, taarifa za kamati ya kidhibiti UKIMWI, taarifa za Kamati ya maadili na taarifa za Kamati ya fedha na Uongozi.Imeandaliwa na:Kitengo Cha Habari na Uhusiano.Manispaa ya Kinondoni. BARAZA LA MADIWANI KINONDONI LAPITISHA TAARIFA YA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO Posted On: January 7th, 2021 Baraza hilo chini ya Mwe... + Read more »