Top ad

Top ad

KITUO CHA KILIMO MALOLO KWA KUSHIRIKIANA NA KITUO CHA UTAFITI WA

 KILIMO TARI-MIKOCHENI WASHIRIKIANA KATIKA KUFANYA UTAFITI WA KILIMO

 CHA MBOGA MBOGA



 

 Akizindua rasimi shughuli hiyo iliyofanyika katika kituo cha kilimo Malolo kilichopo ndani ya Manispaa ya Kinondoni, Dr Zuberi Bira ambaye ni mkuu wa kituo cha utafiti wa kilimo kilichopo Mikocheni (TARI-Mikocheni) amesema utafiti huu ni mwanzo mzuri kuelekea hatua ya kubaini namna nzuri ya kuwa na kilimo bora  cha mboga mboga, aina madhubuti itakiwayo na kupata mboga mahususi zitakazoendana na mahitaji ya walaji kulingana na maeneo yao.





"Kila kitu huenda kwa hatua, Hapa walipofikia Malolo na Manispaa ya Kindoni ni mwendelezo mzuri wa kufikia malengo waliyojiwekea katika kufanya kilimo bora cha Mijini nasi pia kushirikiana nao kwa kila hatua." Dr Bira.



Aidha Afisa kilimo wa Manispaa ya Kinondoni Ndugu Salehe Hija amesema kuwa utafiti huu ni mwendelezo wa mikakati iliyowekwa na kituo cha Malolo ya kuhakikisha kinawanufaisha Wananchi na Wakazi wa Kinondoni kwa ujumla.

Aina 22 ya mboga mboga za mchicha zimefanyiwa utafiti.  Wakulima kutoka Manispaa ya Kinondoni na Ubungo wamehudhuria katika zoezi hilo ambapo awali wamesikiliza semina fupi iliyowasilishwa na Dr Minja katika kuweka bayana nini hasa lengo la utafiti huo, zoezi hilo pia limehusisha uoanjaji wa aina mbalimbali za mchicha ili kubaini upi una ladha nzuri.


Imeandaliwa na
Kitengo cha Habari
na Uhsiano Manispaa ya Kinondoni.


0 comments:

Post a Comment

 
Top