KINONDONI YAZINDUA KAMATI YA MAAFA YA WILAYA. Posted On: November 22nd, 2018 Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Mh Daniel Chongolo leo, amezindua kamati ya maafa ya Wilaya yenye wajumbe 29 ambapo wajumbe 18 ni kutoka timu ya Manispaa na wajumbe 11 ni wadau kutoka nje ya Halmashauri, hafla iliyofanyika katika ukumbi wa Mikutano wa Manispaa. Akizindua kamati hiyo, Mkuu huyo wa Wilaya katika hotuba yake amesema, maafa ni tukio kubwa linalotokea na kuathiri utaratibu wa maisha ya jamii na kusababisha madhara makubwa kwa watu, mali, uchumi na mazingira ambapo huzidi uwezo wa jamii kukabiliana nalo. Ameongeza kuwa kwa Serikali kutambua uwepo wa maafa na majanga Nchini na umuhimu wa kukabiliana nayo, imetunga sheria ya usimamizi wa maafa namba 7 ya mwaka 2015, inayotaka uundwaji wa kamati ufanyike, kwa lengo la kuchukua hatua za kujiepusha nayo na kukabiliana pindi yanapojitokeza. Amesema "Kamati ninayoizindua leo ni utekelezaji wa matakwa ya Sheria, hivyo hatupo hapa kwa bahati mbaya na kamati hii inatambulika kwa mujibu wa sheria tajwa, kifungu cha 15 na 16 hivyo nendeni mkafanye kazi" Amesisitiza Chongolo. Awali akisoma taarifa ya uundaji wa kamati ya usimamizi wa Maafa wa Wilaya kwa niaba ya Mkurugenzi wa Manispaa, Mratibu wa Maafa wa Manispaa hiyo Bi.Pendo Fred amewataja wajumbe wanaounda kamati kuwa ni wakuu wa idara na vitengo 16 vya Manispaa, Jeshi la zimamoto na uokozi Mkoa wa Kinondoni, TARURA, TANESCO, DART, DAWASCO na vyombo vya habari. Aidha ameainisha mipango na mikakati ya kamati kwa mwaka 2018/2019 kuwa ni kufanya mkutano na wadau, kutoa mafunzo kwa kamati za maafa ndani ya Mtaa na Kata, kuanzisha program ya kutoa mafunzo katika jamii na Halmashauri kutekeleza miradi ya DMDP kwa kujenga barabara zenye mifereji. Naye mratibu wa timu ya wataalam ya uokoaji ya Mkoa wa Dar es Salaam (DARMAERT), Ndg Christopher Mzava, alipokuwa akitoa taarifa yake ameyaainisha majukumu ya kamati iliyozinduliwa kuwa ni kuhuisha masuala ya dharura na maafa katika mipango ya maendeleo, kufuatilia tishio la majanga na maafa na kufanya uchunguzi wa kutokea kwa maafa na uchoraji wa ramani. Nyingine ni kuainisha mahitaji ya mafunzo kwa umma na kutoa elimu, kutafuta rasilimali na kusimamia operesheni za maafa na kuunda timu ya ukabilianaji wa maafa na muundo wa kulinda jamii. Uzinduzi wa kamati hiyo pia umehudhuriwa na wawakilishi kutoka Bank ya Dunia, msalaba mwekundu, wawakilishi kutoka ofisi ya Mkuu wa mkoa na waheshimiwa madiwani. Imeandaliwa na Kitengo cha Habari na Uhusiano. Manispaa ya Kinondoni. KINONDONI YAZINDUA KAMATI YA MAAFA YA WILAYA. Posted On: November 22nd, 2018 Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Mh Daniel Chongolo leo, amezi... + Read more »
BARAZA LA MADIWANI MANISPAA YA KINONDONI LAMPONGEZA MKURUGENZI KWA UTENDAJI. Posted On: November 21st, 2018 Baraza la Madiwani Manispaa ya Kinondoni, chini ya Mwenyekiti wake Mh.Benjamini Sitta, kupitia mkutano wake wa Mwaka uliofanyika leo limempongeza Mkurugenzi wa Manispaa hiyo, Ndg Aron Kagurumjuli, pamoja na timu yake nzima kwa utendaji mzuri na ushirikiano mkubwa katika kukusanya mapato, uliopelekea ongezeko la ukusanyaji wake kufikia asilimia 98%. kwa tathmini ya bajeti ya mwaka 2017/2018. Pongezi hizo zimekuja mara baada ya Mkurugenzi huyo kuwasilisha taarifa za utekelezaji wa miradi ya maendeleo, taarifa za utendaji kazi, taarifa za mali za Halmashauri pamoja na tathmini ya bajeti ya mwaka 2017/2018, iliyoonesha kiasi cha bajeti iliyotengwa, makusanyo kutoka vyanzo vya ndani, mapato pamoja na matumizi, huku ikionesha changamoto na mikakati ya kukabiliana nayo katika suala zima la ukusanyaji wa mapato. Amezitaja changamoto hizo kuwa ni baadhi ya vyanzo vikubwa vya mapato kuondolewa katika Halmashauri na kupelekwa Serikali kuu, sheria ndogo zinazotumika kutoza ushuru kwenye masoko kupitwa na wakati, kuwepo mikataba isiyozingatia maslahi ya Halmashauri, na kuwepo migogoro ya vibanda katika masoko na maeneo ya wazi. Aidha Mkurugenzi huyo pia ameainisha mikakati ya kukabiliana na changamoto hizo kuwa ni kuziba pengo la vyanzo vya mapato lililofutwa kwa kuanzisha daftari la walipakodi, kuwepo mchakato wa sheria ndogo zilizopitwa na wakati kufanyika upya, kutambua maeneo ya wazi na vibanda vya biashara vilivyopo katika maeneo ya Umma na kisimamia utozaji wake, kuimarisha mfumo wa upatikanaji wa takwimu za walipakodi na kufanya mapitio ya mikataba ya sasa ya uwekezaji. Katika hatua nyingine katibu Tawala wa Wilaya ya Kinondoni Bi Stella Msofe, katika kikao hicho, amemtangaza rasmi Diwani wa Kata ya Kigogo Mh Mangalu George Manyama kuwa Naibu Meya wa Manispaa hiyo, kwa awamu nyingine tena. Imeandaliwa na Kitengo cha Uhusiano na habari. Manispaa ya Kinondoni. BARAZA LA MADIWANI MANISPAA YA KINONDONI LAMPONGEZA MKURUGENZI KWA UTENDAJI. Posted On: November 21st, 2018 Baraza la Madiwani Manispa... + Read more »
TAMISEMI YAENDESHA MAFUNZO YA SIKU MOJA KWA KAMATI YA LISHE KINONDONI Posted On: November 16th, 2018 NI KUHUSIANA NA UANDAAJI WA MIPANGO YA HUDUMA ZA LISHE KWA MWAKA WA FEDHA 2019/2020. Ofisi ya Raisi -TAMISEMI kupitia kitengo cha lishe imeendesha mafunzo kwa Kamati ya lishe ya Manispaa ya Kinondoni, yahusuyo mipango ya utekelezaji wa huduma za lishe kwa watoto umri chini ya miaka mitano, ikiwa ni pamoja na kuongeza uelewa katika swala zima la utekelezaji wake, hasa uwekaji wa vipaumbele katika bajeti ya 2019/2020. Akifungua mafunzo hayo ya siku moja yaliyofanyika katika ukumbi wa Mikutano wa Manispaa, kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Katibu Tawala wa Wilaya hiyo, Bi Stella Msofe amesema mafunzo haya ni muhimu, na yakawe chachu ya utekelezaji wa jambo hili, hasa ikizingatiwa azma ya Serikali ni kuhakikisha inaepukana na madhara yanayoweza kutokea kwa watoto wetu pindi wanakosa lishe bora Naye mkufunzi kutoka ofisi ya Rais -TAMISEMI Bi.Mary Kibona, alipokuwa akiwasilisha mada ihusianayo na mpango mkakati wa utekelezaji,amefafanua maana halisi ya lishe kuwa ni mchakato wa tangu chakula kinapoliwa mdomoni, kinasagwa na kuingia mwilini na kuanisha madhara ayapatayo mtoto anapokosa lishe bora kuwa ni kupata upungufu wa madini na Vitamini mwilini. Akiainisha mafanikio ya Kamati ya lishe kwa Manispaa ya kinondoni tangu kuundwa kwake, Afisa lishe wa Manispaa hiyo Bi Emiliana Sumaye amesema , kamati hiyo imefanikiwa kupeleka shughuli za lishe kwa idara mtambuka, imefanikiwa kukaa vikao vitatu vya kujadiliana mwelekeo mzima wa lishe na kuainisha njia sahihi za kuhakikisha lengo linafikiwa, imefanikiwa pia kuhakikisha vituo 65 vya kutolea huduma za afya vilivyoko Manispaa vinatoa elimu ya lishe, na kufikia wazazi takribani 19,399 kwa elimu hiyo ya lishe kwa watoto na wajawazito. Pia ameainisha changamoto zinazowakabili kuwa ni Jamii kushindwa kutumia huduma ya uzazi kikamilifu, watoa huduma kutowajibika ipasavyo, kuwepo na upungufu wa watoa huduma ngazi ya jamii, na watoa huduma kutopata elimu ya utoaji wa vidonge vya folic Acidi. Mafunzo haya yaliyohudhuriwa pia na wawakilishi kutoka Ofisi ya Mkoa wa Dar es salaam Bi Janeth Mzava, Mwakilishi kutoka, UNICEF Bi.Joyce Ndeba, Mwenyekiti wa huduma za Uchumi Afya na Elimu Mh.Thadei Masawe, kamati ya lishe ya Manispaa, pamoja na wakuu wa idara na vitengo, yamejadili mada zihusuzo uwasilishaji wa taarifa za utekelezaji wa shughuli za lishe. Nyingine ni Mpango na bajeti ya lishe kwa kutumia planrep, shughuli za lishe/afua za lishe zinazoweza kupangwa ngazi ya vituo vya afya na upatikanaji wa rasilimali watu na fedha. Imeandaliwa na, Kitengo cha Habari na Uhusiano. Manispaa ya Kinondoni. TAMISEMI YAENDESHA MAFUNZO YA SIKU MOJA KWA KAMATI YA LISHE KINONDONI Posted On: November 16th, 2018 NI KUHUSIANA NA UANDAAJI WA MIPAN... + Read more »
KINONDONI KUVITAMBUA, KUVISAJILI NA KUVISIMAMIA VITUO 444 VYA BODABODA NA BAJAJI KATIKA MAENEO YAO Posted On: November 15th, 2018 Manispaa ya Kinondoni imedhamiria kuboresha chanzo cha mapato kitokanacho na vituo vya bodaboda na bajaji kwa kuhakikisha inavitambua, inavisajili na kuvisimamia vituo takribani 444, vilivyopo katika Kata na Mitaa ya Manispaa hiyo kwa kuzingatia,miongozo sheria, kanuni na taratibu zinazoelekeza kufanya hivyo. Akitoa muongozo wa zoezi zima la utambuzi huo, katika mkutano wake na madereva wa bodaboda na bajaji uliofanyika katika ukumbi wa King Solomon leo, Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Mh.Daniel Chongolo amesema, kwa kushirikiana na wakala wa barabara za mijini na vijijini TARURA kwa Manispaa ya Kinondoni, wanatakiwa kuhakikisha suala hilo la utambuzi linafanyika kwa umakini,na wakati, ikiwa ni pamoja na kusimamia tozo zao zitakazokuwa zikitolewa kwa mujibu wa sheria. "Manispaa ya Kinondoni, TARURA, itisheni kikao cha Uongozi wa Wilaya, kaeni nao, kubalianeni taratibu nzuri za kuendesha vikundi vyao, vitambueni, visajilini, na mvisimamie tozo zao."Amesisitiza Chongolo. Awali akitoa taarifa ya vituo hivyo vya bodaboda na bajaji, Mwenyekiti wao ndugu Festo Swai, amesema upo umoja wao uitwao CMPD, ulionzishwa kwa lengo la kusaidiana na kushughulikia changamoto zinazowakabili wao kama vikundi vidogo vidogo, zikiwemo kutosajiliwa na kutambuliwa, kutopatiwa mikopo ya vijana, kutozijua haki zao pindi wanapokutwa na kosa la barabarani, kuuwawa na kuporwa mali zao, pamoja na kupatiwa njia ya kusafirisha abiria mjini. Akijibu swali linalomtaka bodaboda au bajaji kupelekwa mahabusu pindi afanyapo kosa kwa niaba ya OCD Kinondoni, Inspekta Serengeti amesema, dereva wa bajaji au bodaboda kufanya kazi zake bila kuwa na leseni na viambata vyote atakiwavyo kuwanavyo dereva , atashitakiwa kwa kosa la usalama barabarani. Naye Afisa Maendeleo ya Jamii anayehusika na Mikopo, Bi Florah Msilu, katika kufafanua suala la mikopo kwa vijana amesema, kwa mwaka wa fedha 2017/2018, Kinondoni imetenga takribani bilioni 2.7, kwa ajili ya mikopo, na kuwataka vijana wenye umri kuanzia miaka 18-35, katika vikundi kuchangamkia fursa hiyo. Huu ni Mkutano wa kwanza wa Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni kukutana na madereva wa bodaboda na bajaji, pamoja na viongozi wao na kufanya nao mazungumzo ikiwa ni pamoja na kusikiliza kero na changamoto walizonazo. Imeandaliwa na Kitengo cha Uhusiano na habari. Manispaa ya Kinondoni. KINONDONI KUVITAMBUA, KUVISAJILI NA KUVISIMAMIA VITUO 444 VYA BODABODA NA BAJAJI KATIKA MAENEO YAO Posted On: November 15th, 2018 Manis... + Read more »
NILAZIMA MUWE WASIMAMIZI WA JUMLA WA SHUGHULI ZA SERIKALI KATIKA MAENEO YENU" Posted On: November 1st, 2018 Ni agizo lake Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Mh.Daniel Chongolo alipokuwa akiongea na Maafisa Ugani wa Kata ya Bunju katika ziara yake aliyoifanya leo. Amesema Maafisa ugani, watendaji wa Kata na Mitaa katika maeneo yao wanatakiwa kuhakikisha wanawajibika ipasavyo ili kero za wananchi zinazowakabili zitatuliwe kwa ufanisi, umakini, na usawa utakaoleta tija iliyokusudiwa. "Kutenda haki kunajengwa kwa kutimiza wajibu, nilazima muwe wasimamizi wajumla wa shughuli za Serikali katika maeneo yenu, ikiwa ni pamoja na kutoa huduma stahiki kwa wananchi" Amesisitiza Mh.Chongolo. Akisoma taarifa za Kata ya Bunju kwa Mkuu wa Wilaya, Mtendaji wa Kata hiyo Bw.Ibrahim Mabewa amesema Kata yake inamitaa 6, ambayo ni Bunju A, Mkoani, Dovya, Kilungule, Boko, na Basihaya na idadi ya watu kuwa takribani 63,248, na hii ni kwa mujibu wa sensa ya mwaka 2012. Aidha amezitaja changamoto zinazoikabili Kata hiyo ya Bunju kuwa ni Uchimbaji wa kokoto na vifusi, Uchimbaji holela wa mchanga maeneo ya Nyakasangwe, Dampo la taka kuwa mbali na mrundikano wa takataka. Aidha, Mkuu huyo wa Wilaya ameupongeza uongozi mzima wa Halmashauri kwa ufaulu wa asilimia 95.7, matokeo ya darasa la saba kwa mwaka 2018, uliopelekea Kinondoni kuwa ya kwanza kimkoa, na ya tatu kitaifa. Katika ziara yake hiyo, Mkuu huyo wa Wilaya alitembelea maeneo ya shule ya msingi Mkoani, soko la Bunju A, mifereji ya Basi haya, na baadae kufanya mkutano wa hadhara na wananchi katika viwanja vya shule ya Bunju, kwa lengo la kusikiliza kero zao na kuzipatia majibu. Imeandaliwa na Kitengo cha Habari na Uhusiano. Manispaa ya Kinondoni. NILAZIMA MUWE WASIMAMIZI WA JUMLA WA SHUGHULI ZA SERIKALI KATIKA MAENEO YENU" Posted On: November 1st, 2018 Ni agizo lake Mkuu wa ... + Read more »
DC KINONDONI ATOA SIKU SABA KWA WAKANDARASI WA TAKA KUBORESHA HUDUMA HIYO Posted On: November 7th, 2018 NI KUFUATIA KUKITHIRI KWA MALALAMIKO YA WANANCHI KUHUSIANA NA TAKA ZILIZORUNDIKANA MITAANI. Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Mh.Daniel Chongolo ametoa siku saba kwa wakandarasi wa huduma ya kuzoa taka pamoja na Manispaa kuhakikisha wanaboresha utoaji wa huduma hiyo kwenye mitaa husika ili kuondokana na kero inayowasumbua wananchi ya mrundikano wa matakataka. Ametoa agizo hilo leo alipokuwa katika mkutano wa hadhara na wananchi wa Kijitonyama uliofanyika katika viwanja vya shule ya msingi Kijitonyama kisiwani kwa lengo la kusikiliza kero zao na kuzipatia majibu. Amesema iwapo wananchi wanachangia fedha zao kwa ajili ya huduma hiyo, nilazima waipate, kwani kukithiri kwa matakataka mitaani kwaweza kuleta magonjwa ya mlipuko yanayotokana na uchafu. "Natoa agizo, kufika siku ya Jumanne kuanzia leo, kuwe na mwelekeo madhubuti wa kutoa taka kwenye Kata na Mitaa yetu" Ameagiza Chongolo. Akitoa ufafanuzi wa swala hilo, Ndg Peter Abilu ambaye pia ni Afisa Usafishaji wa Manispaa hiyo amesema, kwa sasa Manispaa ya Kinondoni kwa kushirikiana na Maafisa watendaji wa Kata na Mitaa, pamoja na Wakandarasi wa kuzoa taka tumeandaa mpango mkakati utakaoondoa kero hiyo na mazingira kubaki masafi. Awali akitoa taarifa ya Kata ya Kijitonyama kwa Mkuu huyo wa Wilaya, Mtendaji wa Kata hiyo Bi.Elizabeth Minga amesema Kata yake inajumla ya Mitaa Nane, shule za Msingi 7, Sekondari 4, vituo vya polisi 3, Zahanati 2, Masoko 3, Hotel 18, Nyumba za kulala wageni 31, na Bar 50. Aidha ameainisha changamoto kubwa zinazowakabili katika Kata hiyo kuwa ni wananchi kujimilikisha maeneo ya wazi, ujenzi juu ya mifereji na pembezoni mwa kingo, na uthibiti wa taka ngumu. Akipokea maagizo na maelekezo ya Mkuu wa Wilaya, kwa niaba ya Mkurugenzi wa Manispaa, Ndg Maduhu Kazi ambaye pia ni Afisa Mipangomiji ameahidi kuyafanyia kazi maagizo na maelekezo yote yaliyotolewa, ikiwa ni pamoja na kutatua kero zinazowakabili wananchi. Hii ni ziara yake ya pili ambapo ametembelea na kukagua miradi inayotekelezwa katika kata ya Kijitonyama, na kufanya mkutano wa hadhara uliohudhuriwa na wananchi, wakuu wa idara na vitengo pamoja na viongozi mbalimbali wa Kata na Taasisi za Serikali ambapo ziara yake ya kwanza ilifanyika katika kata ya Bunju. Imeandaliwa na Kitengo cha Habari na Uhusiano. Manispaa ya Kinondoni. DC KINONDONI ATOA SIKU SABA KWA WAKANDARASI WA TAKA KUBORESHA HUDUMA HIYO Posted On: November 7th, 2018 NI KUFUATIA KUKITHIRI KWA MALAL... + Read more »
KITUO CHA KILIMO MALOLO KWA KUSHIRIKIANA NA KITUO CHA UTAFITI WA KILIMO TARI-MIKOCHENI WASHIRIKIANA KATIKA KUFANYA UTAFITI WA KILIMO CHA MBOGA MBOGA Akizindua rasimi shughuli hiyo iliyofanyika katika kituo cha kilimo Malolo kilichopo ndani ya Manispaa ya Kinondoni, Dr Zuberi Bira ambaye ni mkuu wa kituo cha utafiti wa kilimo kilichopo Mikocheni (TARI-Mikocheni) amesema utafiti huu ni mwanzo mzuri kuelekea hatua ya kubaini namna nzuri ya kuwa na kilimo bora cha mboga mboga, aina madhubuti itakiwayo na kupata mboga mahususi zitakazoendana na mahitaji ya walaji kulingana na maeneo yao. "Kila kitu huenda kwa hatua, Hapa walipofikia Malolo na Manispaa ya Kindoni ni mwendelezo mzuri wa kufikia malengo waliyojiwekea katika kufanya kilimo bora cha Mijini nasi pia kushirikiana nao kwa kila hatua." Dr Bira. Aidha Afisa kilimo wa Manispaa ya Kinondoni Ndugu Salehe Hija amesema kuwa utafiti huu ni mwendelezo wa mikakati iliyowekwa na kituo cha Malolo ya kuhakikisha kinawanufaisha Wananchi na Wakazi wa Kinondoni kwa ujumla. Aina 22 ya mboga mboga za mchicha zimefanyiwa utafiti. Wakulima kutoka Manispaa ya Kinondoni na Ubungo wamehudhuria katika zoezi hilo ambapo awali wamesikiliza semina fupi iliyowasilishwa na Dr Minja katika kuweka bayana nini hasa lengo la utafiti huo, zoezi hilo pia limehusisha uoanjaji wa aina mbalimbali za mchicha ili kubaini upi una ladha nzuri. Imeandaliwa na Kitengo cha Habari na Uhsiano Manispaa ya Kinondoni. KITUO CHA KILIMO MALOLO KWA KUSHIRIKIANA NA KITUO CHA UTAFITI WA KILIMO TARI-MIKOCHENI WASHIRIKIANA KATIKA KUFANYA UTAFITI WA KILIMO C... + Read more »