JAMII YA KINONDONI YATAKIWA KUJENGA UTAMADUNI WA KUTUMIA MAZIWA ILI KUIMARISHA AFYA YA MWILI NA AKILI KUELEKEA UCHUMI WA KATI WA VIWANDA Posted On: May 24th, 2019 Kauli hiyo imetolewa leo na Mhe Diwani wa kata ya Kunduchi Mh. Michael Urio kwenye hafla ya uzinduzi wa wiki ya unywaji wa maziwa mashuleni inayoratibiwa na Idara ya mifugo na uvuvi kwa Manispaa ya Kinondoni na kufanyika katika Shule ya Sekondari Kondo. Amesema kuwa, serikali ya awamu ya tano inayo nia madhubuti na mwelekeo wa dhati katika kuijenga Tanzania ya Viwanda na uchumi wa Kati, hivyo inahitaji jamii ya watu wenye afya thabiti na akili ya kupambanua mambo kwa ufasaha ili waweze kuendana na sera hiyo. "Maziwa yana virutubisho vyote mhimu vinavyotakiwa katika ujenzi wa mwili na akili hivyo badala ya kunywa pombe na vinywaji vingine tunyweni maziwa kwa wingi ili kuunga juhudi za serikali pia viwanda vyetu vya ndani" ameongeza mhe Urio. Aidha Quenter Mawinda kwa niaba ya msajili wa bodi ya maziwa amewashauri wanafunzi kutumia maziwa kwa wingi ili kuimarisha afya ya akili na mwili na waweze kuendana na Kasi ya Mhe Rais maana anahitaji vijana wachapakazi walioimara. Mara baada ya uzinduzi huo , Manispaa ya Kinondoni kupitia idara ya mifugo na uvuvi imegawa maziwa katika shule tano za Sekondari ambazo ni Shule ya Sekondari Mbopo, Kondo, Mtakuja Beach, Boko na Bunju A, ambapo zaidi ya paketi 350 kwa kila shule zimegawiwa, lakini siku ya pili kwa idadi ya paketi hizo hizo itagawiwa kwa Shule tano za Msingi za Manispaa ya Kinondoni . Uzinduzi huu unatarajiwa kitaifa kufanyika Mkoani Arusha kuanzia tar 28 mwezi wa tano hadi tarehe 1 mwezi wa sita. Imeandaliwa na Kitengo Cha Habari na Uhusiano Manispaa ya Kinondoni. JAMII YA KINONDONI YATAKIWA KUJENGA UTAMADUNI WA KUTUMIA MAZIWA ILI KUIMARISHA AFYA YA MWILI NA AKILI KUELEKEA UCHUMI WA KATI WA VIWANDA ... + Read more »
KAMATI YA SIASA YA MKOA WA DAR ES SALAAM, YARIDHISHWA NA UBORESHAJI WA MIUNDOMBINU YA BARABARA KATIKA WILAYA YA KINONDONI. Posted On: May 24th, 2019 Kamati hiyo Chini ya mwenyekiti wake Bi Kate Kamba imeonesha kuridhishwa na maboresho ya miundombinu ya barabara yanayofanyika maeneo ya katikati hususan Tandale, Kijitonyama na Mwananyamala Manispaa ya Kinondoni. Hali hiyo imedhihirika wakati wa ukaguzi wa miradi hiyo ukiendelea katika ziara ya Kamati ya katika Manispaa ya Kinondoni, chini ya Mwenyekiti wake Bi. Kate Kamba, iliyofanyika kwa lengo la kujiridhisha na utekelezaji wa ilani unaoenda sambamba na ubora wa miradi inayotekelezwa. Bi Kate amesema kuwa wakati umefika sasa kwa Kinondoni kuelekeza nguvu katika kuboresha makazi holela wanayoishi wananchi kwani wanaamini maboresho ya miundombinu yakienda sambamba na maboresho ya makazi ndipo tija itakapopatokana. Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi wa Manispaa hiyo Bw Maduhu Kazi ameishukuru Kamati hiyo kwa kutembelea Kinondoni na kuahidi kufanyia kazi ushauri na maelekezo yote yaliyotolewa na Kamati hiyo ya Siasa. Miradi iliyotembelewa katika ziara hiyo ni pamoja na miradi ya barabara, Shule za Msingi na Sekondari, zahanati pamoja na vituo vya Afya. Imeandaliwa na Kitengo Cha Habari na Uhusiano Manispaa ya Kinondoni. KAMATI YA SIASA YA MKOA WA DAR ES SALAAM, YARIDHISHWA NA UBORESHAJI WA MIUNDOMBINU YA BARABARA KATIKA WILAYA YA KINONDONI. Posted On: May... + Read more »
JAMII YA KINONDONI IMETAKIWA KUSHIRIKI KATIKA UBORESHAJI WA MIUNDOMBINU PAMOJA NA MAZINGIRA YA SHULE ILI WANAFUNZI WAWEZE KUPATIWA ELIMU BORA. Posted On: May 7th, 2019 Kauli hiyo imetolewa leo na Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Mh Daniel Chongolo katika hafla ya upokeaji mabati kutoka kampuni ya ando, yatakayowezesha kuezeka darasa moja katika shule ya msingi Wazo hill. Amesema kwa juhudi za pamoja kati ya Serikali kwa kushirikiana na wadau katika kuhakikisha miundombinu ya shule, elimu na mazingira vinaboreshwa, kwa hakika taaluma katika Wilaya yeu itapanda. "Serikali inalengo mahususi la kuhakikisha miundombinu ya elimu inapatikana na inaboreshwa, katika hili ninafurahishwa sana kuona tunao wadau katika Wilaya yetu walio tayari kutuunga mkono, tunawashukuru sana kwa uzalendo mlionao"Amesema Chongolo. Kwa upande wake Mkurugenzi wa kampuni ya (ando), Bw Godlistern Maimu amesema, kampuni yao imejiwekea utaratibu wa kusaidia jamii kwani wanaamini ndoto za wanafunzi zitafikiwa pale watakapopatiwa elimu bora na katika mazingira mazuri. Naye Afisa Elimu wa Manispaa hiyo Ndg Kiduma Mageni alipotakiwa kuongea, aliushukuru uongozi mzima wa kampuni ya ando) kwa kushirikiana na Serikali katika kuboresha mazingira ya elimu, na kuahidi kuyalinda na kuyatumia kwa makusudi yaliyokusudiwa. Katika hatua nyingine Mhe Chongolo ameahidi kutatua changamoto ya vyumba vya madarasa pamoja na ukosefu wa ofisi ya walimu unaoikabili shule ya Msingi Wazo hill kwani kwa sasa ina idadi ya wanafunzi zaidi ya 3000 huku ikiwa na walimu 57 pekee. Imeandaliwa na Kitengo Cha Habari na Uhusiano Manispaa ya Kinondoni. JAMII YA KINONDONI IMETAKIWA KUSHIRIKI KATIKA UBORESHAJI WA MIUNDOMBINU PAMOJA NA MAZINGIRA YA SHULE ILI WANAFUNZI WAWEZE KUPATIWA ELIMU BO... + Read more »
WITO WATOLEWA KWA WAZAZI NA WALIMU WA SHULE ZA SERIKALI MANISPAA YA KINONDONI. NI KATIKA MWENDELEZO WA UTEKELEZAJI WA MPANGO WA MITIHANI YA PAMOJA KWA WANAFUNZI WA DARASA LA SABA. Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni kupitia idara ya elimu Msingi imeendelea na mpango wa kuandaa mitihani ya pamoja kwa wanafunzi Wa darasa la saba, ambapo leo imetangaza matokeo ya mtihani wa jaribio la pamoja uliofanyika tarehe 02-03/05/2019. Akitangaza matokeo hayo kwa niaba ya Afisa Elimu Msingi Bi Fatuma Mwiru, amewasihi Walimu na Wazazi wa shule za serikali kutilia mkazo fursa hii kwani ni maandilizi sahihi na kipimo tosha kuelekea mtihani wa Taifa. Ametoa nasaha hiyo baada ya kubaini kuwa idadi ya wanafunzi waliofanya vizuri na kupata zawadi imetawaliwa na watoto kutoka shule binafsi. "Napenda kuwasihi Wazazi na Walimu Wa shule za serikali wawe msitali wa mbele kuhakikisha watoto wanafanya vizuri katika mitihani hii maana ni dira tosha kuelekea mtihani wa Taifa" ameongeza Bi Fatuma. Aidha Bi Fatuma amesema kuwa ofisi ya Mkurugenzi kupitia idara ya Elimu Msingi ipo bega kwa bega kuhakikisha matokeo chanya yatapatikana katika mtihani wa Taifa na ndio maana Zawadi zinatolewa kwa wanaofanya vizuri ili kuleta hamasa kwa wanafunzi kusoma kwa bidii. Akitangaza matokeo hayo, amesema jumla ya wanafunzi 270 walifanya jaribio hilo la pamoja ambapo waliopata daraja A ni wanafunzi 112, daraja B ni wanafunzi 150 na daraja C ni wanafunzi 08. Katika hatua nyingine Bi Fatuma amekiri kuwa ushindani ni wa hali ya juu sana maana mtoto aliyeongoza mtihani uliopita amekosekana kumi bora lakini aliyeongoza leo mtihani uliopita hakuwepo kumi bora. Imeandaliwa na Kitengo Cha Habari na Uhusiano Manispaa ya Kinondoni. WITO WATOLEWA KWA WAZAZI NA WALIMU WA SHULE ZA SERIKALI MANISPAA YA KINONDONI. NI KATIKA MWENDELEZO WA UTEKELEZAJI WA MPANGO WA MITIHANI ... + Read more »
KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU KINONDONI, YATAKIWA KUBUNI MBINU MBADALA ZA KUONGEZA VYANZO VYA MAPATO KATIKA HALMASHAURI YAO Ushauri huo umetolewa leo na Mstahiki Meya wa Manispaa hiyo Mh.Benjamini Sitta katika kikao cha majumuisho ya ziara hiyo baada ya kutembelea miradi ya elimu kilichofanyika katika ukumbi w mikutano wa Manispaa. Amesema kamati ya huduma za uchumi, afya na elimu ndio injini ya Halmashuri kwani inagusa sekta muhimu za uchumi na afya ambazo moja kati yake isipoenda sawia basi hakuwezi kuwa na mafanikio. Amesema" Hii kamati ya Huduma za Uchumi ni ya muhimu sana, lakini mmejikita sana kwenye miradi ya elimu, mnasahau sekta muhimu ya uchumi na afya, mimi nadhani wakati umefika sasa muje na mikakati mipya ya kukuza uchumi kwa kuibua vyanzo vipya vya mapato" Mh Sitta. Akipokea ushauri huo kutoka kwa mstahiki Meya, Mwenyekiti wa Kamati hiyo Mhe. Thadeus Massawe ameahidi kuufanyia kazi, yeye pamoja na timu yake nzima, na kumshukuru Mstahiki Meya kwa ushauri huo wenye tija kwa Halmashauri yetu. Kamati hiyo katika ziara yake, imetembelea na kukagua miradi mitatu ya shule ambayo ni ; shule ya Msingi na awali Liberman iliyopo Kawe, Shule ya awali Del Paul iliyopo Wazo na Shule ya awali Mbweni Heights iliyopo Mbweni. Imeandaliwa na Kitengo Cha Habari na Uhusiano Manispaa ya Kinondoni. KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU KINONDONI, YATAKIWA KUBUNI MBINU MBADALA ZA KUONGEZA VYANZO VYA MAPATO KATIKA HALMASHAURI YAO Us... + Read more »
MKUU WA MKOA WA DAR ES SALAAM, MH.PAUL MAKONDA AFANYA ZIARA KATIKA WILAYA YA KINONDONI KUKAGUA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO. Posted On: April 15th, 2019 Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Mhe Paul Makonda leo amefanya ziara katika wilaya ya Kinondoni kukagua miradi ya maendeleo inayotekelezwa kwa fedha kutoka serikali kuu ,Mapato ya ndani ya Manispaa na fedha za wadau wa nje na ndani ili kujiridhisha kwa kulinganisha taarifa anazopewa na hali halisi katika maeneo ya mradi husika ambapo pamoja na kupongeza hatua zilizofikiwa katika utekelezaji wa Miradi hiyo ametoa Maagizo na maelekezo mbalimbali yanayotakiwa kufanyiwa kazi ili kuboresha na kuifanya iendane na thamani halisi. Katika mradi wa ujenzi wa soko la magomeni Mhe. Mkuu wa mkoa alionesha kutoridhishwa na ubadilishaji wa dizaini ya ujenzi wa Soko hilo, hivyo amewataka Wahandisi na Wataalam wengine wanaosimamia Miradi mbalimbali ya ujenzi kutokubali Wahandisi washauri wa miradi kubadilisha dizaini ya miradi hiyo, kwani inaweza kupoteza ubora na kutoa huduma kwa wachache tofauti na lengo la serikali la kuangalia mahitaji ya sasa na baadae. Akiwa katika kituo cha Afya Kigogo, Mhe.Mkuu wa Mkoa pamoja na kuupongeza uongozi wa wa Manispaa ya Kinondoni kwa maamuzi ya busara ya kununua majengo, kuyakarabati na kujenga majengo mengine kwa matumizi ya Kituo kikubwa cha Afya kitakachohudumia zaidi ya wakazi laki moja, ameagiza kasi ya utekelezaji wake iongezwe na endapo kutakuwa na jambo linalokwamisha kuhusiana na ufuatiliaji katika Mamlaka za juu ashirikishwe Mkuu wa Wilaya kwani heshima ya Serikali kutaka kupata matokeo ya Mradi kwa wakati na sio ugumu wa kupata matokeo ya miradi inayotekelezwa. Mhe Mkuu wa mkoa alieleza kutoridhishwa na baadhi ya Barabara zinazojengwa chini ya kiwango hususani Barabara ya Mburahati ambapo pamoja na Mkandarasi kuwa nyuma ya muda wa Utekelezaji, viwango vya ubora wake sio wa kuridhisha katika upana na ubora wa mifereji ya maji ya mvua, hivyo amewataka wasimamizi wa mradi huo kuhakikisha wanafanyia kazi ili kuiwezesha kuwa katika viwango vinavyokubalika. Akizungumzia gharama za ujenzi wa miradi ya barabra hizo, Mhe. Mkuu wa Mkoa amezitaka Mamlaka husika kuliangalia suala la tofauti ya gharama za ujenzi kwa Miradi ya Barabara ya DMDP inayojengwa kwa thamani ya bilioni 2 kwa kilometa moja na zile za TANROAD na TARURA zikijengwa kwa thamani ya bilioni 1.3 kwa kilometa moja, kwani tofauti ni kubwa na fedha zinazotumika katika ujenzi ni mkopo sio msaada, hivyo akashauri kuliangalia jambo hili. Katika hatua nyingine Mhe. Mkuu wa Mkoa amemuagiza Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Mhe. Daniel Chongolo kushughulikia malalamiko ya vibarua wanaodai kupunjwa malipo yao na kampuni za ujenzi ambazo huwalipa shilingi 7500 kwa siku badala ya shilingi 12,500 kwa siku zinazotakiwa kulipwa kisheria. Katika hatua nyingine Mhe. Mkuu wa Mkoa ameshauri Fedha zilizotakiwa kutumika katika ujenzi wa kipande cha mita 200 katika Barabara ya Simu 2000 na nyingine zikajenge Barabara ya Shekilango Ubungo maziwa kupita Makaburi ya Urafiki ili kuondoa kero kwa watumiaji wa Barabara hiyo. Akiwa katika Mradi wa ujenzi wa soko la Sinza II Kata ya kijitonyama ambapo linajengwa kwa gharama ya milioni 128 zinazotokana na mapato ya ndani ya Manispaa, Mhe. Mkuu wa Mkoa amefurahishwa na Ubora wake na kutaka likamilishwe haraka na kuwaweka wafanyabiashara sambamba na kuboresha maeneo ya maegesho na njia ya kuingilia Magari Sokoni hapo. Aidha katika ziara hiyo Mhe Mkuu wa Mkoa alionesha kusikitishwa kwake na baadhi ya maeneo kuwa na mazingira machafu hivyo ameuagiza uongozi wa Manispaa kuhakikisha Maafisa Watendaji wa Kata katika maeneneo hayo kuanza kujitathmini uwezo wao katika kusimamia usafi kwani kama Watendaji Wakuu wa Maeneo husika wana wajibu wa kuwasimamia Maafisa Afya wa Kata kutekeleza kikamilifu Majukumu yao. Mwisho Mhe. Mkuu wa Mkoa amewataka wakandarasi wa Kampuni ya Scoll na Del-monte waliosimamishwa kupewa miradi ya ujenzi katika Mkoa wa Dar es salaam kwa kosa la kujenga Barabra chini ya kiwango, kuzijenga upya kwa gharama zao kama walivyoagizwa haraka iwezekanavyo ili waweze kupewa miradi mingine ambapo amempongeza Mkandarasi wa kampuni ya Delmonte anayerudia ujenzi katika barabara ya Mabatini kwa gharama zake na kwa kiwango cha kuridhisha. IMEANDALIWA NA KITENGO CHA MAWASILIANO NA UHUSIANO MANISPAA YA KINONDONI. MKUU WA MKOA WA DAR ES SALAAM, MH.PAUL MAKONDA AFANYA ZIARA KATIKA WILAYA YA KINONDONI KUKAGUA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO. Posted... + Read more »
TATHMINI YA MATOKEO YA MTIHANI WA KWANZA WA UTAMILIFU (MOCK) DARASA LA SABA KINONDONI YATOLEWA Posted On: April 12th, 2019 Akitoa tathmini hiyo leo, Afisa elimu msingi Manispaa ya Kinondoni Bw.Kiduma Mageni amesema, jumla ya shule 138, zenye wanafunzi 12, 622, walifanya mtihani huo ambao ni sawa na asilimia 99.33% na kati yake waliofaulu ni 9,302, sawa na asilimia 74.20% Amesema lengo la mtihani huu ni kutekeleza mkakati maalum wa kuhakikisha inaendelea kufanya vizuri kitaaluma hasa ikizingatiwa Kinondoni ilishika nafasi ya tatu Kimkoa kwa ufaulu wa asilimia 95.70%, matokeo ya mtihani wa kumaliza elimu ya msingi (PSLE) 2018. "Kinondoni iliandaa mkakati maalumu wa kuendelea kufanya vizuri zaidi kitaaluma kwa kuhakikisha inaendesha mitihani miwili ya utamilifu kiwilaya kwa wanafunzi wa darasa la saba 2019 na mtihani huo ulifanyika tarehe 27-28/03/2019" Amefafanua Mageni. Aidha amezitaja shule tatu za serikali zilizofanya vizuri kuwa ni Msisiri, Victoria na Lugalo na shule za binafsi ni Royal Elite, Mother's of Mercy na Libermann. Amewataka walimu kutumia Matokeo haya kama chachu ya kurekebisha changamoto ndogondogo zilizoonekana ili kuweza kufanya vizuri mitihani ijayo ya ngazi ya Mkoa na Taifa. Katika hafla hiyo iliyofanyika katika ukumbi wa Oysterbay na kuenda sambamba na ugawaji zawadi kwa shule zilizofanya,vizuri kutoka CRDB Bank, pia imehudhuriwa na waalimu wakuu, waratibu wa Elimu Kata pamoja na waalimu wa darasa la saba. Imeandaliwa na Kitengo Cha Habari na Uhusiano Manispaa ya Kinondoni. TATHMINI YA MATOKEO YA MTIHANI WA KWANZA WA UTAMILIFU (MOCK) DARASA LA SABA KINONDONI YATOLEWA Posted On: April 12th, 2019 Akitoa tathm... + Read more »