Top ad

Top ad





Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni awataka Maafisa watendaji wa Kata kuimarisha ulinzi na usalama katika Kata zao, kuhakikisha wanafanya vikao na wanachi wao, na kutoa taarifa za mapato na matumizi kwenye Kata., kutokujihusisha na uuzaji wa maeneo, kuhakikisha kunakuwepo na mpango kazi unaoeleweka na kufuatwa kwa kila wiki, na kutenga siku ya kusikiliza kero za wanachi,

Ameyasema hayo alipokuwa katika ziara yake Kata ya Tandale kwa lengo la kupata taarifa za Kata, mafanikio na Changamoto zake.

Mkuu wa Wilaya pia ametembelea maeneo ya Soko la Tandale, shule ya Msingi Muhalitani kuona uchakavu wa vyumba vya madarasa, mradi wa maji uitwao “maji yetu” uliofadhiliwa na EU, Kingdom of Beligium pamoja na Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania , ujenzi wa barabara na kituo cha watoto yatima kilichoko tandale.

 

0 comments:

Post a Comment

 
Top