KINONDONI YASAINI MIKATABA NA MAKAMPUNI MAWILI YA TAKRIBANI BILIONI 58 Posted On: June 13th, 2019 NI KWA AJILI YA UJENZI NA MABORESHO YA MTO NG'OMBE NA BARABARA YA SHEKILANGO KWA KIWANGO CHA NJIA NNE. Akisaini mikataba hiyo, kati yake na makampuni hayo, Mkurugenzi wa Manispaa ya Kinondoni Ndg. Aron Kagurumjuli amesema, mradi wa mto ng'ombe utakaogharimu bilioni 32, utajengwa na kampuni ya China Henan International Cooperation Group CO. LTD na mradi wa barabara ya shekilango wa njia nne utakaogharimu shilingi 26 bilioni, utajengwa na Kampuni ya China road and bridge Cooperation hali itakayosaidia si tu kuboresha maeneo hayo bali pia kuyapandisha hadhi kwa kiwango kusudiwa. Amesema katika mikataba hiyo pia yatajengwa mabwawa ya kukusanyia maji eneo la karibu na chuo cha maji kutoka maeneo mbalimbali na maji hayo yataruhusiwa kuingia taratibu mto ng'ombe hali ambayo itasaidia kupunguza mafuriko. Akishuhudia utilianaji sahihi mikataba hiyo, Mstahiki Meya Wa Manispaa ya Kinondoni Mhe. Benjamini Sitta amesema, Serikali ya awamu ya tano ni Serikali sikivu yenye lengo la kuboresha makazi duni na kuwatoa wananchi kwenye kifungo cha mateso ya mafuriko, na ujenzi huu wa mto ng'ombe utasaidia kwa kiasi kikubwa kupunguza kadhia hiyo iliyokuwa ikisumbua wananchi wa maeneo ya Tandale na kijitonyama. Aidha Meya Sitta pia amewataka makandarasi wanaojenga miradi hiyo kujenga kwa wakati na kwa ubora stahiki ili waweze kumaliza kero iliyokuwa inawasumbua wananchi kwa muda mrefu. Imeandaliwa na Kitengo Cha Habari na Uhusiano Manispaa ya Kinondoni. KINONDONI YASAINI MIKATABA NA MAKAMPUNI MAWILI YA TAKRIBANI BILIONI 58 Posted On: June 13th, 2019 NI KWA AJILI YA UJENZI NA MABORESHO Y... + Read more »
ELIMU YA AFYA, UZAZI NA UPIMAJI NA USHAURI NASAHA KWA WANANCHI YATOLEWA KINONDONI. Posted On: June 7th, 2019 Kinondoni kwa kushirikiana na shirika lisilo la kiserikali la JHPIEGO lenye kauli mbiu ya "TUPANGE PAMOJA"yaendesha zoezi la utoaji elimu ya Afya ya Uzazi, upimaji na ushauri nasaha kwa wananchi ili kulinda na kuboresha afya zao. Akifafanua kuhusu zoezi hilo, lililofanyika katika mtaa wa Hananasif Kinondoni, Mganga Mkuu wa Manispaa hiyo Dr Festo Ndugange amesema kuwa kipaumbele cha serikali ya awamu ya tano ni kujenga na kukuza uchumi wa nchi kupitia Viwanda, katika kuhakikisha hilo linatimia wanahitajika watu wenye afya njema kimwili na kiakili ili waweze kutoa mchango utakiwao kwa wakati sahihi. "Wakati viongozi wetu wanapigania masuala ya kukuza uchumi wanahitaji mwitikio chanya kutoka kwenye jamii na hilo linawezekana endapo jamii hiyo itakuwa na watu wenye afya njema na nguvu imara, nasi tumeona namna nzuri ya kutoa mchango wetu ni kuwapa elimu, kinga na tiba imara wakati wote" ameongeza Dr Festo. Akiongea katika zoezi hilo, mratibu wa huduma ya afya ya uzazi na mtoto Manispaa ya Kinondoni Bi. Edith Manase Mboga amesema, huduma na elimu inayotolewa inalenga kupunguza au kumaliza kabisa matatizo yanayoikumba jamii hasa ikizingatiwa chanzo chake ni ukosefu wa uelewa na kutokuwa na uthubutu wa familia kukaa na kuweka mikakati ya pamoja juu ya masuala ya afya. Huduma walizopatiwa wananchi hao ni elimu juu ya afya ya uzazi, upimaji wa saratani ya shingo ya kizazi na matiti, shinikizo la damu, ushauri nasaha na upimaji wa hiari wa VVU. Wananchi waliojitokeza katika zoezi hilo wameishukuru Manispaa ya Kinondoni kwa fursa hiyo adimu itakayowawezesha kupata elimu juu ya mwasuala ya Afya ya uzazi pamoja na athari azipatazo mtu asiyefuata masuala hayo ya Afya. Imeandaliwa na Kitengo Cha Habari na Uhusiano Manispaa ya Kinondoni. ELIMU YA AFYA, UZAZI NA UPIMAJI NA USHAURI NASAHA KWA WANANCHI YATOLEWA KINONDONI. Posted On: June 7th, 2019 Kinondoni kwa kushirikiana... + Read more »
ELIMU YA AFYA, UZAZI NA UPIMAJI NA USHAURI NASAHA KWA WANANCHI YATOLEWA KINONDONI. Posted On: June 7th, 2019 Kinondoni kwa kushirikiana na shirika lisilo la kiserikali la JHPIEGO lenye kauli mbiu ya "TUPANGE PAMOJA"yaendesha zoezi la utoaji elimu ya Afya ya Uzazi, upimaji na ushauri nasaha kwa wananchi ili kulinda na kuboresha afya zao. Akifafanua kuhusu zoezi hilo, lililofanyika katika mtaa wa Hananasif Kinondoni, Mganga Mkuu wa Manispaa hiyo Dr Festo Ndugange amesema kuwa kipaumbele cha serikali ya awamu ya tano ni kujenga na kukuza uchumi wa nchi kupitia Viwanda, katika kuhakikisha hilo linatimia wanahitajika watu wenye afya njema kimwili na kiakili ili waweze kutoa mchango utakiwao kwa wakati sahihi. "Wakati viongozi wetu wanapigania masuala ya kukuza uchumi wanahitaji mwitikio chanya kutoka kwenye jamii na hilo linawezekana endapo jamii hiyo itakuwa na watu wenye afya njema na nguvu imara, nasi tumeona namna nzuri ya kutoa mchango wetu ni kuwapa elimu, kinga na tiba imara wakati wote" ameongeza Dr Festo. Akiongea katika zoezi hilo, mratibu wa huduma ya afya ya uzazi na mtoto Manispaa ya Kinondoni Bi. Edith Manase Mboga amesema, huduma na elimu inayotolewa inalenga kupunguza au kumaliza kabisa matatizo yanayoikumba jamii hasa ikizingatiwa chanzo chake ni ukosefu wa uelewa na kutokuwa na uthubutu wa familia kukaa na kuweka mikakati ya pamoja juu ya masuala ya afya. Huduma walizopatiwa wananchi hao ni elimu juu ya afya ya uzazi, upimaji wa saratani ya shingo ya kizazi na matiti, shinikizo la damu, ushauri nasaha na upimaji wa hiari wa VVU. Wananchi waliojitokeza katika zoezi hilo wameishukuru Manispaa ya Kinondoni kwa fursa hiyo adimu itakayowawezesha kupata elimu juu ya mwasuala ya Afya ya uzazi pamoja na athari azipatazo mtu asiyefuata masuala hayo ya Afya. Imeandaliwa na Kitengo Cha Habari na Uhusiano Manispaa ya Kinondoni. ELIMU YA AFYA, UZAZI NA UPIMAJI NA USHAURI NASAHA KWA WANANCHI YATOLEWA KINONDONI. Posted On: June 7th, 2019 Kinondoni kwa kushirikiana... + Read more »
WADAU NA JAMII KWA UJUMLA WAMETAKIWA KUONESHA UPENDO KWA KUWAKUMBUKA NA KUWAJALI WATU WENYE UHITAJI MAALUMU KATIKA JAMII. Posted On: May 31st, 2019 Hayo yamebainika leo wakati Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Mhe.Daniel Chongolo kwa kushirikiana na asas ya Human releif foundation walipozuru katika kituo cha watoto yatima cha Kijiji cha Furaha kilichopo Mbweni na kutoa msaada wa sukari, unga, mafuta ya kupikia na mchele kwa kituo hicho. Amesema ni jukumu letu kuhakikisha watoto hawa wanapatiwa upendo unaostahili ikiwemo haki za kisheria za watoto ambazo ni kulindwa, kusikilizwa, kupatiwa elimu, makazi na malazi. Amesema "Watoto hawa ni jukumu letu sote, lazima tuwapende na kuwajali, kwani jamii yetu imezungukwa na watu mbalimbali wanaohitaji kutazamwa kwa jicho la tatu kama vile watoto yatima na wengineo, hivyo ni wajibu wetu kuwapatia vitu wanavyohitaji".Mhe. Chongolo Ameongeza kuwa kilichofanywa leo na Mr Mbarak F.Baghumesh kutoka asas ya Human Releif Foundation ni ishara kubwa ya upendo na inatakiwa kuigwa na kila mtu, kwani hata yeye hajaangalia dini yake isipokuwa ametanguliza upendo na uthamani wa kiutu. Aidha ameahidi kushirikiana bega kwa bega na wadau wengine katika kuhakikisha changamoto mbalimbali zinazoikabiri taasisi ya Kijji cha Furaha zinatatuliwa na kuwataka watu wa idara ya ustawi wa jamii Manispaa ya Kinondoni kutafuta njia mbadala za kuwasaidia watoto yatima wanaomaliza shule katika vituo mbalimbali. Kwa upande wake Mr Mbarak ambaye ni Operation Manager wa shirika la Human Relief Foundation, amesema kuwa mbali na kutoa msaada hui, ataendelea kushirikiana na ofisi ya Mkuu wa Wilaya katika kuwathamini watu wenye mahitaji maalum bila kujali rangi wala dini zao. Imeandaliwa na Kitengo Cha Habari na Uhusiano Manispaa ya Kinondoni. WADAU NA JAMII KWA UJUMLA WAMETAKIWA KUONESHA UPENDO KWA KUWAKUMBUKA NA KUWAJALI WATU WENYE UHITAJI MAALUMU KATIKA JAMII. Posted On: May ... + Read more »
DC KINONDONI AKEMEA VIKALI WAKANDARASI WAZEMBE Posted On: May 31st, 2019 NI WALE WASIOFANYA KAZI ZAO KWA WELEDI, HALI INAYOPELEKEA UCHELEWESHWAJI WA UKAMILISHAJI WA MIRADI YA MAENDELEO. Kauli hiyo imetolewa leo, na Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Mhe Daniel Chongolo katika ziara yake ya ukaguzi wa utekelezaji wa miradi ya maendeleo ili kujiridhisha na hatua za utekelezaji zilizofikiwa. Amesema wakandarasi ni lazima waelewe umuhimu wa kutekeleza na kukamilisha miradi hii kwa mujibu wa makubaliano na mikataba waliyoingia kwani kwa kutokufanya hivyo kunarudisha nyuma maendeleo na ni kutoitendea haki si tu Serikali bali hata wananchi walengwa wa mradi unaotekelezwa. Aidha Mhe. Chongolo ameonesha kutoridhishwa na kasi ya ujenzi wa kiwanda cha kuchakata taka kinachojengwa na mkandarasi wa Kampuni ya CRJE East Africa LTD kwani katika kipindi Cha miezi 11 ya mkataba wake mradi huo umekamilika kwa asilimia 20 pekee na huku akiwa amebakiwa na miezi 7 ya kumaliza mkataba. Amesema "wakandarasi Kama hao hawatavumiliwa katika Wilaya yangu na endapo itafika tarehe 30 mwezi June bila kuonesha dalili za mabadiliko ya mradi huo mkandarasi huyu achukuliwe hatua sitahiki.", Mh. Chongolo. Kadhalika amekemea tabia ya baadhi ya wakandarasi wakubwa kuchukua tenda za Ujenzi na baadae kuwapa kandarasi wengine au wadogo kuifanya kazi hiyo, huku wao wakibaki kuwa kama madalali. Katika hatua nyingine amewataka watendaji wa Kata kusimamia kwa ukaribu miradi hiyo ili iweze kukamilika kwa wakati na iweze kuleta tija kwa jamii Miradi iliyotembelewa na Mkuu wa wilaya leo ni pamoja na Barabara ya Tegeta nyuki, Barabara ya Boko Magereza, Hospitali ya Wilaya ya Mabwepande, Shule ya wasichana ya Mabwe Tumaini girls, Kiwanda cha kuchakata taka kilichopo Mabwepande na Shule ya wavulana ya Mbweni Teta. Imeandaliwa na Kitengo Cha Habari na Uhusiano Manispaa ya Kinondoni. DC KINONDONI AKEMEA VIKALI WAKANDARASI WAZEMBE Posted On: May 31st, 2019 NI WALE WASIOFANYA KAZI ZAO KWA WELEDI, HALI INAYOPELEKEA UCHE... + Read more »
KOREA YA KUSINI YARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MKATABA WA MAHUSIANO KATI YAKE NA MKOA WA DAR ES SALAAM Posted On: May 30th, 2019 NI ULE WA MIAKA MITATU UNAOHUSU KUWAJENGEA UWEZO WATAALAM WA KILIMO KATIKA MATUMIZI YA TEKNOLOJIA ZA KILIMO CHA MJINI CHA KISASA . Korea ya Kusini jimbo la Gyeongsanam imeoneshwa kuridhishwa na utekelezaji wa makubaliano yalioingiwa kati yake na Mkoa wa Dar és salaam, yahusuyo utoaji wa huduma ya mafunzo ya kuwajengea uwezo wataalam wa kilimo, kuhusiana na teknolojia za Kilimo chá kisasa cha mjini ili kukabiliana na changamoto zilizopo kama ufinyu wa ardhi na magonjwa ya mimea. Hayo yamedhihirika leo wakati wa hafla fupi ya mapokezi ya ujumbe kutoka korea ya kusini, waliozuru kwa lengo la kufanya majadiliano ya namna ya kuingia upya mkataba mwingine, wenye lengo la kuboresha zaidi sekta hiyo ya kilimo hasa upande wa matumizi ya teknolojia ya vifaa vya kisasa kwa matumizi madogo ya ardhi yenye tija, baada ya ule wa awali kuisha. Akipokea ujumbe huo kutoka Korea ya Kusini, ulipozuru kituo cha kilimo Malolo Kinondoni, Mstahiki Meya wa Manispaa hiyo, Mhe. Benjamin Sitta amesema Dar es salaam hususani Kinondoni leo imefungua ukurasa mpya wa maendeleo katika sekta ya kilimo cha mjini kwani mkataba huo uliodumu kwa miaka mitatu umeibua ari mpya ya maendeleo na kuleta mapinduzi katika sekta hii kwa kuiniua pato lá mkulima pindi atumiapo utaalam huo ulio rahisi na wamatumizi madogo ya eneo. "Hakika mapinduzi ya kilimo cha mjini yameneemeshwa vilivyo kupitia uhusiano wetu na Korea kusini maana tumejifunza mambo mengi sana kupitia wao na tunaamini hatutaishia hapa tutaenda mbele zaidi"ameeleza Msitahiki Meya. Naye Kaimu Katibu Tawala Msaidizi Uchumi na Uzalishaji wa Mkoa Dar es salaam Dkt. Elizabeth Mshote amesema kuwa Manispaa za jiji la Dar es salaam zimenufaika vilivyo kupitia uhusiano huo na Korea kusini na kuanishia kuwa awamu ijayo itakuwa nzuri zaidi kwani ushiriki utajikita zaidi katika miundombinu ya kilimo tofauti na ule wa awali uliokuwa na lengo la kujengea uwezo wataalam hao wa kilimo. Kwa upande wao Mr. Lee, Do Wan ambaye ni Mkurugenzi wa Division ya Ushirikiano na nchi za nje kutoka Jimbo la Gyeongsangnam na Dkt Lim Chae Shin kutoka Kituo cha mafunzo ya technologia ya kisasa ya kilimo ATEC kilichopo Mjini Jinju Korea kusini, amesema kuwa anaamini Tanzania inaweza kabisa kufikia Korea kusini maana mwitikio uliooneshwa ndani ya miaka mitatu ni wa kipekee sana na unadhirisha hamu ya mapinduzi ya kilimo ndani ya mioyo yao. Hafla hiyo imeshirikisha wataalamu wa sekta ya kilimo kutoka Halmashauri zote tano za mkoa wa Dar es salaam, pamoja na KOICA. Imeandaliwa na Kitengo cha Habari na Uhusiano Manispaa ya Kinondoni. KOREA YA KUSINI YARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MKATABA WA MAHUSIANO KATI YAKE NA MKOA WA DAR ES SALAAM Posted On: May 30th, 2019 NI ULE... + Read more »
KINONDONI YAENDESHA SEMINA ELEKEZI KWA WENYEVITI NA MAKATIBU WA KAMATI ZA USIMAMIZI WA MAAFA ZA KATA. Posted On: May 25th, 2019 NI KUHUSIANA NA UTEKELEZAJI WA SHERIA YA MAAFA YA MWAKA 2015 NA JINSI YA KUKABILIANA NA MAJANGA KATIKA SEKTA HIYO. Akifungua semina hiyo leo katika ukumbi wa DMDP jijini Dar es salaam, Mkuu wa idara ya Mendeleo ya Jamii Bi.Halima Kahema amesema, lengo ni kuzijengea uwezo kamati za kata kwani ndio msingi mzima katika kutekeleza sera na usimamizi wa sheria hii ya maafa ya mwaka 2015, ngazi ya Kata na Mitaa. Ameongeza kuwa ili uweze kutekeleza Jambo ni lazima ulijue, na katika hili ni dhahiri kabisa mana kunapokosekana usimamizi mzuri unaoenda sambamba na utekelezaji wowote wa sheria hakika zoezi linakuwa gumu, na hata uchukuaji wa hatua stahiki katika sekta hiyo pia unakuwa mgumu. Bi. Halima amesema "wenyeviti na makatibu wa Kamati mnatakiwa kwanza kuijua sheria vizuri ili muweze kuwa na maamuzi na mamlaka kamili katika kutafuta njia nzuri zaidi za kukabiliana na maafa pale yatakapojitokeza". Aidha mratibu wa Maafa Manispaa ya Kinondon Bi. Pendo Mwaisaka wakati akiongea,ametoa msisitizo wa utoaji wa taarifa kwa wakati, na taarifa hizo ziambatane na takwimu sahihi la tukio husika na kusisitiza kuwa suala la Maafa ni suala mtambuka linalohitaji nguvu ya pamoja na Serikali, sekta binafsi na wadau wengine. Mada zilizowasilishwa katika semina hiyo ni Mpango wa kukabiliana na dharura mkoa wa Dar es salaam, Jinsi ya kuandaa mipango ya kujiandaa na kupunguza athari za majanga, Uokozi na namna ya kukabiliana na majanga mbalimbali, maafa, majanga na uokozi na nini kifanyike kukabiliana na majanga. Nyingine ni miradi inayotekelezwa na Manispaa ya Kinondoni DMDP iliyolenga kupunguza athari za mafuriko, sheria ya usimamizi ya maafa ya mwaka 2015 pamoja na utoaji wa taarifa za majanga. Semina hii imepata uwakilishi kutoka DarMAERT, oxford policy, Chama cha msalaba mwekundu, na Jeshi la zimamoto, na kuhudhuriwa na maafisa watendaji wa kata, maafisa maendeleo ya jamii Kata pamoja na wadau wengine. Imeandaliwa na Kitengo Cha Habari na Uhusiano Manispaa ya Kinondoni. KINONDONI YAENDESHA SEMINA ELEKEZI KWA WENYEVITI NA MAKATIBU WA KAMATI ZA USIMAMIZI WA MAAFA ZA KATA. Posted On: May 25th, 2019 NI KUHU... + Read more »